Ticker

10/recent/ticker-posts

NDOA YA MWIGIZAJI SHAMSA FORD YAVUNJIKA 'DICK AMENINYANYASA NA KUNIPIGA KWA MUDA MREFU ILA NILIFICHA KUEPUKA AIBU''

Staa  mrembo kutoka Bongo Movies, Shamsa Ford amefunguka rasmi kuhusu kuvunjika kwa ndoa yake ya kimila aliyofunga na mwanaume wake wa siku nyingi, Dickson ‘Dick’ akikiri kuwa amepoteza muda mwingi kwa mtu ambaye hakuwa na mapenzi ya dhati kwake.

Akizungumza  na gazeti la Ijumaa Wikienda, Shamsa alitiririka kwamba mara nyingi alikuwa akichezea kichapo tena akiwa na ujauzito wa miezi minne wa mtoto wao, Terry lakini kipindi chote hicho alikuwa akivumilia ili kukwepa aibu na kumlindia heshima.

“Dick ameninyanyasa kwa muda mrefu  lakini kuepuka aibu ya kuwa mastaa hawatulii, nikawa navumilia kipigo kikali hivyo niliamua kuachana naye tangu Oktoba, mwaka jana na sikutaka kusema ila sasa nimeweka wazi kutokana na yeye kuanika mambo yetu kwenye mtandao wa kijamii,” alisema Shamsa.
Alipotafutwa Dick, simu yake iliita bila kupokelewa hivyo jitihada za kumpata zinaendelea

Post a Comment

0 Comments