Ticker

10/recent/ticker-posts

Waziri Jerry Silaa Achangia Milioni 44 Ujenzi wa Kanisa Katoliki

 

Mbunge wa jimbo la Ukonga na waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya Makazi Mhe.Jerry Silaa kupitia wadau wake mbali mbali amechangia kiasi cha shilingi milioni 44.8 kwa ajili ya ujenzi wa Parokia katika jimbo ka Ukonga.

Silaa amekabidhi kiasi hicho kwa Waziri Mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mhe.Kasim Majaliwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe.Edward Mpogolo mara baada mbio za hisani kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa kanisa Parokia ya Pugu.