Shirika
la Nyumba la Taifa (NHC) limemtaka Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima,
Askofu Josephat Gwajima, kuhamisha makazi ya kanisa lake lililopo
katika viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar es Salaam leo.
Meneja
Uhusiano wa NHC, Yahya Charahani amelieleza Gazeti la Nipashe kuwa,
walimpatia notisi Askofu Gwajima ya kuhama eneo hilo mwezi mmoja
uliopita, lakini hakutekeleza badala yake ameendelea kulitumia eneo hilo
kuendesha shughuli za kanisa lake, zikiwamo ibada.
Charahani
alisema eneo hilo ni mali ya NHC na ni maalum kwa ajili ya ujenzi wa
mji wa kisasa na wakazi waliokuwa wanaishi eneo hilo walishalipwa fidia
muda mrefu uliopita ili kuondoka.
“Lile
eneo ni la NHC kwa muda mrefu na kabla ya hapo kulikuwa na nyumba
nyingi sana na zilibomolewa, hizo zilizobaki zimebaki tu kimakosa,” alisema Charahani.
Aliongeza kuwa, hiyo siyo mara ya kwanza kwa NHC kumpatia notisi Askofu kiongozi huyo kulihamisha kanisa lake.
Kwa
mujibu wa Charahani, NHC walimpatia notisi Askofu Gwajima ya mwezi
mmoja kuondoka katika makazi hayo na kwamba notisi hiyo ilimalizika
Machi 9, mwaka huu.
Alisema baada ya kumalizika kwa notisi hiyo, NHC lilimpatia muda zaidi Askofu huyo ambao unamalizika leo.
Juhusi
za kumpata Askofu Gwajima kuthibitisha kama amepokea notisi hiyo
zilishindikana kutoka na simu yake ya mkononi kutopatikana kila
alipopigiwa tangu Alhamisi iliyopita.
Hata
hivyo, jana alipotafutwa Mwanasheria wa Askofu Gwajima, Paul Mallya
kuelezea hatua ya NHC ya kumpa mteja wake notisi ya kuhamisha makao ya
kanisa lake, alisema bado hajapata notisi hiyo.
“Sijapata taarifa hiyo, ndiyo kwanza nasikia kwako, ngoja nifuatilie nije nikupe majibu yaliyokamilika,” alisema Mallya.
Mpekuzi blog
0 Comments