Labda
tunajisifu kuwa tuko kwenye ulimwengu ambao teknolojia imerahisisha
vingi.. unahitaji kuwasiliana na mtu yuko mbali.. Viber, Facebook,
Twitter zinasaidisa yaani kirahisi kabisa.
Kutokana na Sheria za nchi kuwa tofauti,
hii story ya Marekani kuruhusu mtu kuomba talaka kwa kutumia message ya
Facebook imenishtua kidogo.
Ishu
ilianzia utata ulioanza mapema kabisa Ellanora Baidoo alipofunga ndoa
ya kimila mwaka 2009 na mpenzi wake Victor Sena Blood-Dzraku, lakini
uhusiano wao ukawa kama umevunjika; bwana anaishi mahali ambako bibi
hapajui, mawasiliano yao ni Facebook basi !!
Bibi
akaona isiwe taabu, akaenda Mahakamani kuomba Mahakama impe ruhusa
aombe talaka yake kupitia message ya Facebook kwa kuwa ndio njia pekee
ambayo walikuwa wakitumia kuwasiliana.
Jaji wa Mahakama ya Manhattan aliruhusu bibi huyo abadilishe status yake, aweke #single
halafu huyo bwana afikishiwe ujumbe wa kudai talaka kupitia message ya
Facebook, ambayo toka message hiyo imetumwa jamaa hakujibu.
Wakili wa mwanamke huyo Andrew Spinnell
amefurahishwa na uamuzi huo wa Mahakama, anaamini kwa sasa kuna haja ya
kutumia hata hizi social networks kutoa hukumu kama ilivyofanywa kwa
mume wa Baidoo.
0 Comments