Ticker

10/recent/ticker-posts

Taarifa Muhimu Kutoka Tanesco Kuhusu Umeme Kukosekana Maeneo mbalimbali Leo

 Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetoa taarifa kwa Wateja wake leo August 22,2023 kuwa kumetokea hitilafu ya mfumo katika kituo cha uzalishaji umeme kwa njia ya gesi cha Ubungo II.

“Hitilafu hiyo imesababisha mapungufu ya uzalishaji wa umeme kwa jumla ya megawati 268 kutokuwa kwenye mfumo wa usafirishaji umeme, hivyo baadhi ya maeneo kwenye Mikoa nchini yanakosa huduma ya umeme kwa nyakati tofauti”

“Jitihada za kurekebisha tatizo hilo zinaendelea na tutawataarifu Wateja wetu kila baada ya saa 4 kadri hali ya upatikanaji wa huduma ya umeme itakavyokuwa inaimarika”

“Shirika linawashukuru Wateja wake kwa uvumilivu katika kipindi chote ambacho huduma ya umeme inakosekana”

Post a Comment

0 Comments