Ticker

10/recent/ticker-posts

WAZIRI ANGELLAH KAIRUKI: TARURA KUTUMIA TRILIONI 1.2 KUBORESHA BARABARA NCHINI,MATIVILLA,LONDO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

 

Waziri wa Nchi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Angellah J. Kairuki akizungumza na wafanyakazi wa TAMISEMI na TARURA kabla ya uzinduzi wa Magari 43 ya Makatibu tawala wasaidizi (Miundombinu) pamoja na Mameneja wa TARURA Mikoa na Wilaya leo Makao Makuu ya TARURA eneo la Mtumba Jijini Dodoma.

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) unatarajia kutumia Shilingi Trilioni 1.2 kwa mwaka wa fedha 2023/24 katika kuboresha barabara za vijijini na mijini zenye urefu wa Km 144,429.77 ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya usafiri na usafirishaji kwa urahisi.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Angellah Kairuki wakati wa hafla ya kukabidhi magari kwa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) iliyofanyika katika Ofisi za TARURA Makao Makuu katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Mtendaji Mkuu wa Tarura Mhandisi Victore H. Seff akizungumza na wafanyakazi wa TAMISEMI na TARURA kabla ya uzinduzi wa Magari 43 ya Makatibu tawala wasaidizi (Miundombinu) pamoja na Mameneja wa TARURA Mikoa na Wilaya leo Makao Makuu ya TARURA eneo la Mtumba Jijini Dodoma.

 Mhe. Kairuki amesisitiza kuwa Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kuboresha miundombinu ya barabara za vijijini na mijini kupitia TARURA ili kuhakikisha wananchi wanasafiri kwa urahisi.

’’Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kuwezesha wananchi kuwa kitovu cha maendeleo na kuimarisha ubia baina ya wananchi na Serikali, katika ngazi ya msingi kwa kuimarisha miundombinu ya barabara kupitia TARURA na kwa kufanya hivyo, Bajeti ya TARURA imeongezeka hadi kufikia tilioni 1.2 kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo pia leo tunakabidhi magari yatakayosaidia katika usimamizi wa miradi ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati’’, amesema Mhe. Kairuki .

Mweneyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Dennis Londo (Mb) akizungumza na wafanyakazi wa TAMISEMI na TARURA kabla ya uzinduzi wa Magari 43 ya Makatibu tawala wasaidizi (Miundombinu) pamoja na Mameneja wa TARURA Mikoa na Wilaya leo Makao Makuu ya TARURA eneo la Mtumba Jijini Dodoma.

Aidha, Mhe. Kairuki ametoa pongezi kwa Mtendaji Mkuu wa TARURA Mhandisi Victor H. Seff pamoja na watumishi wote wa TARURA kwa usimamizi bora wa miradi katika maeneo mbalimbali nchini.

Akitoa taarifa fupi ya utekelezaji wa kazi za ujenzi na matengenezo ya barabara za Wilaya hadi kufikia tarehe 30 Juni 2023 Mtendaji Mkuu wa TARURA Mhandisi Victor H. Seff ameeleza kuwa utekelezaji wa kazi umefikia asilimia 85 ambapo jumla ya Shillingi Bilioni 621 zimetumika kati ya Shillingi Billioni 653 zilizopokelewa.

Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu Mhandisi Rogatus Mativilla  akizungumza na wafanyakazi wa TAMISEMI na TARURA kabla ya uzinduzi wa Magari 43 ya Makatibu tawala wasaidizi (Miundombinu) pamoja na Mameneja wa TARURA Mikoa na Wilaya leo Makao Makuu ya TARURA eneo la Mtumba Jijini Dodoma.

Akiongea katika hafla hiyo Naibu katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu Mhandisi Rogatus Hussein Mativila amesema pamoja na kazi nzuri inayofanywa na TARURA na watumishi wake pia  kuna kila sababu ya kumshukuru Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuamua kuiongezea Bajeti TARURA lengo likiwa ni kuhakikisha inatekeleza kazi zake kwa ukubwa hadi ngazi ya chini ili kumfanya mwananchi hasa mkulima aweze kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa haraka na kwa gharama nafuu kwani ukishajenga au kuboresha barabara unakua umeshaboresha thamani ya mazao yao na kazi zao za kujenga uchumi.

Baadhi ya wafanyakazi wa TAMISEMI na TARURA waliohudhuria Hafla ya  uzinduzi wa Magari 43 ya Makatibu tawala wasaidizi (Miundombinu) pamoja na Mameneja wa TARURA Mikoa na Wilaya leo Makao Makuu ya TARURA eneo la Mtumba Jijini Dodoma.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Dennis Londo (Mb)ameipongeza TARURA kwa kazi zinazofanyika katika kuimarisha miundombinu ya barabara na kwamba kazi hizo zinaonekana katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Baadh ya Magari kati ya magari 43 yaliyozinduliwa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Angellah Kairuki Makao Makuu ya TARURA Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma kwa ajili ya Makatibu tawala wasaidizi (Miundombinu) pamoja na Mameneja wa TARURA Mikoa na Wilaya leo
Baadh ya Magari kati ya magari 43 yaliyozinduliwa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Angellah Kairuki Makao Makuu ya TARURA Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma kwa ajili ya Makatibu tawala wasaidizi (Miundombinu) pamoja na Mameneja wa TARURA Mikoa na Wilaya leo.

 

Post a Comment

0 Comments