Hayo yameelezwa na wajumbe wa Kamati hiyo katika kikao cha majumuisho kilichofanyika mkoani Tanga kati ya Kamati ya Ukaguzi pamoja na Meneja wa TARURA Mkoa wa Tanga Mhandisi George Tarimo.
Kamati ilitembelea ujenzi wa daraja la Mkomazi lenye urefu wa mita 40.6 katika barabara ya Kwasunga – Mswaha, ujenzi wa barabara ya Hosana – Lutheran – Mount view kwa kiwango cha lami yenye urefu wa Km 0.73 Km katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, matengenezo ya barabara ya Mkumbi – Muheza Estate kwa kiwango cha lami yenye urefu wa Km 0.675 Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, pamoja na barabara ya Sahare Phase II kiwango cha lami yenye urefu wa Km 0.60 katika Halmashauri ya Jiji la Tanga.
“Tumetembelea miradi katika Halmashauri ya Jiji laTanga, Wilaya ya Muheza, Wilaya ya Korogwe pamoja na mradi mkubwa wa kimkakati wa ujenzi wa daraja la Mkomazi utakaotumia shilingi bilioni 3.8 mpaka kukamilika kwake, tumejionea kazi kubwa iliyofanyika katika Mkoa huu’’, alisema
Mwenyekiti wa Kamati aliendelea kusisitiza kuwa jukumu lao kubwa ni kutoa ushauri kwa yale wanayoyaona ili miradi iweze kuwanufaisha wananchi.
Pia Kamati imeishauri TARURA Mkoa wa Tanga kuendelea kusimamia miradi kwa ukaribu, kufanya usafi katika mitaro, uwekaji wa alama na taa za barabarani pamoja na kuongeza sehemu za watembea kwa miguu katika miradi ya barabara waliyotembelea.
0 Comments