Ticker

10/recent/ticker-posts

TARI YAENDELEA KUTEKEREZA AGIZO LA WAZIRI MKUU UTOAJI MBEGU BORA ZAO LA MCHIKICHI



Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya utafiti wa kilimo nchini TARI dkr Geofrey Mkamilo ambae pia mratibu wa kuamasisha upandaji wa michikichi nchini akikabidhi sehemu ya mbegu za mchikichi zenye uwezo wa kutoa mafuta ya mawese kwa wingi na zinakua kwa muda mfupi ,mbegu hizo zimekabidhiwa elfu hamsini 50,000 kwa SSP Dominic Kazimili ambae ndiye mkuu wa gereza la Kwitanga mkoani kigoma ikiwa njia ya kuteketeza agizo la waziri mkuu katika kupunguza uwagizaji wa mafuta ya kula kutoka nje ya nchi.
Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya utafiti wa kilimo nchini TARI dkr Geofrey Mkamilo akifafanua jambo kwa waandishi wa habari hawapo pichani juu ya mikakati ya kuzalisha mbegu milioni tano ifikapo june 2020 ambapo mpaka sasa wameshazalisha mbegu milioni 1.2 .
Mkurugenzi wa kituo cha utafiti wa michikichi TARI Kihinga Dr Philison Kagimbo anaelezea kitaalamu jinsi ya uzalishaji wa miche ya michikichi ya Tenela yenye uwezo mkubwa katika utoaji wa mafuta ya kula ambapo moja ya mchakato wake ni pamoja uwekwa katika pipa na kufukiwa chini na kuwekewa mkaa ili kupata nyuzi joto 40 kusaidia ukuaji wa miche kwa haraka.

Sehemu ya mbegu 50,000 zilizokabidhiwa na Taasisi ya utafiti wa kilimo TARI kwa gereza la Kwitanga mkoani Kigoma ,ambapo mbali TARI kukabidhi mbegu katika gereza hilo pia ameshakabidhi kwa halmashauri sita za mkoa wa kigoma na jeshi la kujenga taifa JKT Bulombola .


Na Mwandishi Wetu,Kigoma
Wakulima wa michikichi mkoani kigoma wamefuraishwa na hatua  ya serikali kugawa bule mbegu za muda mfupi na zenye tija katika ukamuaji wa mafuta ya mawese ya zao la michikichi aina ya Tenela badala ya mbegu za zamani ambazo utumia zaidi ya miaka kumi mpaka kuanza uzalishaji.
Wakulima hao wamesema  mara baada ya taasisi ya utafiti wa kilimo nchini TARI kugawa zaidi ya mbegu 50,000 katika jeshi la Magereza Kwitanga kwa lengo la kutekeleza agizo la serikali kupitia Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika kuboresha uzalishaji wa zao la mchikichi ili kupunguza tatizo la kuagiza mafuta ya kula kutoka  nje ya nchi
Akikabidhi mbegu hizo kwa maafisa wa jeshi la magereza Kwitanga mkurugenzi mkuu wa TARI Dkr Geofrey Mkamilo amesema wameshaotesha mbegu za kisasa la zao la mchikichiki zaidi ya milioni 1.2 zenye uwezo wa kutoa mafuta kwa wingi na kuota kwa muda mfupi  ambazo zitagaiwa kwa wakulima na taasisi za serikali bule  na zimesaidia kuokoa zaidi ya bilioni 5.4 ambazo zingetumika kununua mbegu hizo.
Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya utafiti wa kilimo nchini TARI dkr Geofrey Mkamilo ambae ndio mratibu wa kuamasisha upandaji wa michikichi nchini amesema Tanzania inahitaji mafuta ya kula tani laki 570 huku yanayozalishwa nchini ni tani laki  205 na kusabaisha kutumia shilingi bilioni 443 kwaajili ya kuagiza tani  laki 365 ili kukidhi hali ya mafuta ya kula hapa nchini.
Ambapo uwoteshaji na Ugawaji wa miche  ya michikichi katika mkoa wa Kigoma kutokana na agizo la waziri mkuu Kassim Majaliwa unaendelea kwa kasi huku wanatarajia mpaka ifikapo June 2020 zaidi ya miche milioni 5 itakuwa imeoteshwa kwaajili ya kupewa wakulima.



from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2Fe0m17
via

Post a Comment

0 Comments