Ticker

10/recent/ticker-posts

DON WILLIAMS ALIYETAMBA NA MUZIKI WA COUNTRY

Na: Moshy Kiyungi,Tabora.
Wale waliokuwa vijana wa miaka ya 1950 hadi na 1990, wanakumbuka burudani za muziki tulivu wa Country toka kwa wanamuziki mbalimbali duniani.
Msomaji wa makala hii nikujuze muziki wa Country kuwa ni aina ya muziki ambao ilikuwa ikifurahiwa sana nchini Marekani kwa miaka mingi iliyopita.
Muziki huo pia una wasikilizaji huko nchini Canada, Uingereza, na sehemu zingine Ulimwenguni. Umaarufu wa muziki wa Country huja na kupotea mithiri ya maji ya bahari ambayo hujaa na kupwa.
“This World is not our home, we are just passing through…” ni kati ya mistari ya wimbo wa Country.
Miongoni mwa wanamuziki maarufu wa muziki huo wa Country ni pamoja na Johnny Cash, Patsy Cline, the Judds, Dolly Parton, Glen Campbell, George Jones na Tammy Wynette, Kenny Rogers, Loretta Lynn, Randy Travis, Don Williams, Tanya Tucker, Willie Nelson, Reba Mc Entire, Garth Brooks na Toby Keith.
Makala haya yanamzungumzia mwanamuziki Don Williams, ambaye alikuwa ni miongoni mwa wanamuziki hao.
Wasifu wa mwanamuziki huyo unaeleza kuwa alizaliwa Mei 27, 1939 katika kitongoji cha Floydada, huko Texas nchini Marekani.
Williams alianza kupiga gitaa kutoka kwa mama yake akiwa kijana. Baadaye aliweza kupiga muziki katika bendi ya Rock n 'roll na Folk ambazo ni za muziki wa Country.
Alikuwa na sauti ya chini, nyororo, tamu na laini, ilipachikwa majina bandia ya "Jitu Pole" la muziki wa Country.
Juhudi zake zilipelekea kuanzisha bendi yake ya kwanza na iitwayo "The Strangers Two".
Mwaka wa 1964 alimwajiri Susan Taylor ambapo walianzisha bendi ya Pozo-Seco Singers.
Bendi hiyo iliingia mkataba na kampuni ya Columbia Records, akaweza kuachia idadi kubwa ya nyimbo takriban hamsini.
Kundi hilo lilivunjika mwaka wa 1971, ambapo Williams akamua  kuimba kibinafsi.
Wimbo wake wa mwaka wa 1974, "We Should Be Together," ulichukua nafasi ya tano, na alitia saini na kampuni ya kurekodi ya ABC / Dot .
Wimbo wake wa kwanza akiwa na ABC / Dot, "I Wouldn't Want to Live If You Didn't Love Me," ulichukua nafasi ya kwanza, na ulikuwa wa kwanza wa msururu wa nyimbo zake zilizovuma za kwanza kumi kati ya mwaka wa 1974 na 1991.
Mwaka wa 1978, Don Williams alikuwa mwanaume muimbaji wa mwaka kwa mujibu wa Shirika la miziki wa Country na wimbo wake "Tulsa Time" ilikuwa wimbo wa mwaka.
Nyimbo zake zimerekodiwa na wasanii kama vile Johnny Cash, Eric Clapton, Lefty Frizzell, Josh Turner, Sonny James, Alison Krauss, Billy Dean, Charley Kiburi, Kenny Rogers, Alan Jackson, Waylon Jennings na Pete Townshend.
Mwanzoni wa mwaka wa 2006, Williams alitangaza "Matembezi yake ya buriani katika Ulimwengu" Aliimba nchini Marekani na nje ya nchi, kumalizia matembezi yake na "Buriani ya mwisho" alifanya huko Memphis, Tennessee katika kituo cha Cannon cha Waimbaji 21 Novemba 2006.
Tukio hilo la mwisho lilipokewa vizuri na kihisia kwa mashabiki waliohudhuria.
Kulingana na wafanyakazi wake, Williams sasa walitamka kuwa amestaafu na hakuna ziara tena, ingawa uwezekano wa kuwepo kwa rekodi mpya.
Don alifunga pingu za maisha na Joy Bucher Aprili 10, 1960, wakabarikiwa kupata watoto wawili, Gary na Tim.
Muziki wake pia ni maarufu kimataifa, ikiwa ni pamoja na Uingereza, Australia.
Mwanamuziki huyo aliiaga dunia Septemba 08, 2017, akiwa amefikisha umri wa miaka 78.
Mungu aipumzishe roho yake pahala pema peponi, Amina.

Mwisho
Mwandaaji wa makala haya anapatikana kwa namba
0767331200, 0736332200, 0784331200 na 0713331200.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2D6zBKX
via

Post a Comment

0 Comments