Ticker

10/recent/ticker-posts

MWINGEREZA AWATAKA MASHABIKI, WASANII NA WADAU KUTHAMINI VYA KWAO.

   
     Na.Khadija seif, Michuzi TV

WAANDAAJI wa filamu nchini wametakiwa kuongeza ufanisi na ujuzi katika kazi zao ili kuboresha na kuingia ushindani katika soko la kimataifa la filamu.

Akizungumza na Michuzi tv Katibu Mtendaji wa Baraza la sanaa nchini (BASATA) Godfrey Mwingereza amesema China imekua nchi yenye ushindani katika kutengeneza filamu zenye ubora kuanzia wachezaji, picha mnato,kiwango cha picha kwa ujumla .

"Ni wazi kwa sasa nchi ya China imekua ikijizolea mashabiki siku hadi siku na kutokana na tamthilia zao kutafsiriwa kwa lugha ya kiswahili inaleta ushawishi na chachu ya kutazama tamthilia hiyo kwa mfano Maododo ilikua ni tamthilia yenye mashabiki wengi nikiwemo mimi mwenyewe,"

Hata hivyo amewapongeza Kampuni ya startimes kwa kuandaa hafla hiyo fupi na kuwaleta nchini wasanii kutoka China waliogiza kwenye tamthilia ya ode to Joy iliyowekwa sauti kwa lugha ya sauti ikiongezwa na mwanadada Andy.

"Hafla Kama hizi ni mojawapo ya fursa kwetu ili kuendelea kujifunza vingi kutoka kwenye tamaduni za wenzetu kwani wanaonyesha jinsi gani wanavothamini wasanii wao na utamaduni wao kwa ujumla, kwani wamejitokeza wachina wengi ukumbini kuwaona wasanii hao hiyo ni dalili tosha ya kuonyesha uthamini wa vya kwao,"
 Meneja Maudhui Zamaradi Nzowa akimkaribisha Katibu Mtendaji Mkuu wa Baraza la Sanaa (BASATA) Godfrey Mwingereza ukumbi wa Kilimanjaro hotel katika hafla ya kuwakaribisha wasanii walioigiza kwenye tamthilia ya ode to Joy
 Kikundi cha ngoma kiitwacho Makumbusho kikitumbuiza katika hafla fupi ya kutambulisha msimu wa pili wa tamthilia ya ode to Joy inayorushwa na King'amuzi cha startimes.
 Katibu Mtendaji Mkuu wa Baraza la sanaa (BASATA) Godfrey Mwingereza akiwa pamoja na wadau mbalimbali wasanaa katika hafla fupi ya kutambulisha msimu wa pili wa tamthilia ya ode to Joy
Jamii ya watu wa nchi ya China waliojitokeza kwenye hafla fupi ya kuwakaribisha wasanii walioigiza kwenye tamthilia ya ode to Joy 


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2MJIUpC
via

Post a Comment

0 Comments