Na Mwandishi Wetu, Arusha
WANARIADHA watakaoshiriki mashindano ya mbio za Nyika za Taifa Februari 16, mwaka huu katika viwanja vya Magereza Moshi, mkoani Kilimanjaro wameahidi kufanya makubwa zaidi.
Kufanya vizuri kwenye mashindano hayo kutawapa fursa ya kushiriki mashindano ya mbio za Nyika za Dunia zinazotarajiwa kufanyika nchini Denmark Machi 30, mwaka huu. Wakizungumza kwenye mazoezi yaliyofanyika viwanja vya Magereza Arusha wanariadha hao walisema chini ya mdhamini wao Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA),wamejaa tumaini la kufanya vizuri zaidi.
Mwanariadha kutoka timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Anjelina Daniel aliwashukuru NCAA kwa kuwadhamini ambapo amekuwa na wakati mzuri zaidi wa kufanya mazoezi. “Ninawaahidi mashindano ya Nyika Moshi nitashika namba ya kwanza hapa nimekuwa wa pili,” alisema Anjelina.
Kaimu Meneja wa Uhusiano NCAA Joyce Mgaya alisema Mamlaka ya Ngorongoro ilitambua fursa ya uzalendo kwenye mchezo huo na mingine.“Hili ni jukwaa linaloweza kutangaza vivutio vya utalii. Tuliona vizuri kuungana na RT kuwatia moyo wachezaji, tunaamini watakuwa mabalozi wazuri wa utalii,” alisema Mgaya.
Naye Katibu Mkuu wa RT Wilhelm Gidabuday aliwashukuru NCAA kwa kuwashika na mkono.
|
Kaimu Meneja wa Mahusiano wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCCA), Joyce Mgaya akizungumza na wanariadha kutoka Kanda ya Kaskazini viwanja vya Magereza mjini Arusha yalipofanyika matayarisho ya kushiriki mbio za Nyika za Taifa mjini Moshi, NCAA wamelifadhili shirikisho hilo
|
Baadhi ya wanariadha wa Kanda ya Kaskazini wakiwa na walimu,mfadhili wao Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), Viongozi wa riadha na Viongozi wa Shirikisho la Riadha (RT) wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa matayari ya kushiriki mbio za Nyika za Taifa yatakayofanyika mjini Moshi Machi mwaka huu.
Mwanariadha kutoka Kanda ya Kaskazini nchini Tanzania akishiriki matayarisho ya mashindano ya mbio za Nyika za Taifa zitakazofanyika viwanja vya Magereza Moshi, mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kuchagua washindi wa kwanza hadi wa Sita watakaounda Timu ya Taifa itakayoshiriki mashindano ya Dunia ya mbio za Nyika Machi 30, mwaka huu nchini Denmark
Wanariadha kutoka Timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), na wengine wakishirikisha matayarisho ya mashindano ya mbio za Nyika za Taifa zitakazofanyika viwanja vya Magereza Moshi, mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kuchagua washindi wa kwanza hadi wa Sita watakaounda Timu ya Taifa itakayoshiriki mashindano ya Dunia ya mbio za Nyika Machi 30, mwaka huu nchini Denmark
Mwanariadha kutoka Kanda ya Kaskazini nchini Tanzania akishiriki matayarisho ya mashindano ya mbio za Nyika za Taifa zitakazofanyika viwanja vya Magereza Moshi, mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kuchagua washindi wa kwanza hadi wa Sita watakaounda Timu ya Taifa itakayoshiriki mashindano ya Dunia ya mbio za Nyika Machi 30, mwaka huu nchini Denmark
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Gidabuday akizungumza na wanahabari katika viwanja vya Magereza mjini Arusha kuhusu umuhimu wa wanariadha nchini kujenga uzalendo wa kushiriki matayarisho ya mashindano ya mbio za Nyika .
|
|
from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2G9qEE6
via
0 Comments