Ticker

10/recent/ticker-posts

ALI KIBA ASEMA DIAMOND AKIMTUMIA PICHA ZA TUZO NAZOWANIA MTV ATAZIPOST INSTAGRAM KUMPA SAPOTI



Ali Kiba amefunguka hayo kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM na B Dozen alipokuwa akifanya mahojiano maalum,alisema kuwa ana washangaa sana baadhi ya mashabiki wanasema kuwa hatoi sapoti kwa baadhi ya wasanii lakini yeye wakati anatoa kava za video yake ya Cheketua aliwatumia baadhi ya wasanii,ambao wapo walipost kwenye akaunti zao za Instagram lakini wengine hawakufanya hivyo lakini hajalalamika.
‘’Kwanza niseme kuwa sina bifu na Diamond na hajanitumia picha nipost kwenye akaunti yangu ya Instagram kama angenitumia ningepost kwani sina tatizo naye,’alisema Ali Kiba
Aidha alisema kuwa yeye amekuwa balozi wa wanyama kupitia kampeni ya wildlife ambaye ni mwakilishi pekee kutoka Tanzania akiwa na mastaa kibao duniani ambao wamejitolea kwenye kampeni hiyo kama Jack Chan,David Beckam,prince William,Leonardo Dicaprio na wengine wengi lakini hakuna msanii aliyempost na kumpongeza kwa kuiwakalisha nchi.
‘’Kumbuka na mimi nipo kwenye kampeni na watu maarufu duniani kwanini watu wachukulie poa? Na wale wanatutetea sisi na wanyama wetu sisi, kwanini watu wanachukulia poa? Wale wazungu wamejitolea na mimi pi nimejitolea watu wanachukulia poa kwanini?,alisema Ali Kiba.
‘Mimi siwezi kusema kama nimelipiza kisasi siwezi.. sipo katika hayo mambo, lakini ‘always’ nakuwa hivyo umenitumia na mimi nakutumia na ukinitumia picha nakusapoti wengi huwa wananitumia picha nawasapoti, Tanzania kuna tabia ya wasanii kutosapotiana watu wanaangalia kitu gani mtu ameharibu siyo kitu gani kimejenga,’aliongeza Ali Kiba.
Akizungumzia suala la uzalendo alisema kuwa siyo kwenye ishu ya kumsapoti Diamond tu ni kusapotiana wasanii wote cha muhimu ni wasanii kukaa kikao cha pamoja na wawepo wadau mbalimbali watoe elimu ya umuhimu wa kuwa wazalendo wa nchi yao.