Leo imetimia miaka mitatu tangu aliekuwa staa nguli wa Bongo Movies,
Steven Kanumba afariki dunia, hizi ni baadhi ya jumbe ambazo mastaa
kutoka Bongo Movies wameziandika kuonyesha kumbukumbu zao kwa staa huyo.
Ni siku ambayo siwezi kusahau maisha yangu yote pumzika kwa amani
kanumba wangu., nilikupenda ila mungu alikupenda zaidi . Pumzika kwa
amani.
Johari
Huwezi kutaja mafanikio ya bongo movies bila kukutaja wewe...tunakuthamini na tunakukumbuka milele
JB
Steven Charles Kanumba pengo lako mpaka leo atujaweza kuliziba na
sidhani kama tutaweza tena ingawa Sasa umetimiza miaka mitatu tangu
ulipotuacha ghafla kiukweli ni ngumu sana kusahau Tutakukumbuka daima
kwani tunapozungumzia kiwanda cha sinema nchini lazima tulitaje jina
lako kaka angu ...R.I.P KANUMBA.
Odama
Ni miaka 3 tangu umeondoka marehemu kanumba.Tulikuhitaji sana but Mungu
alikuhitaji zaidi.ulikuwa una mchango mkubwa sana katika kuipeperusha
bendera ya Tanzania.uliipenda kazi yako toka moyoni kiasi cha kutumia
hata hela ya mfukoni mwako kujitangaza kimataifa.Mungu ailaze roho yako
mahala pema peponi k...TOO PAINFULY
Shamsa ford
Nimiaka mitatu tangu utuache lakini tunaona kamajana Dah hakika pengo
lako haliwezi kuzibika.... Mungu akuweke unapo stahili.... Amin
Riyama
0 Comments