Wakati wakiwa kwenye ziara yao nchini Peru, Nyota wa kundi la One
Direction Zayn Malik na Louis Tomlinson wameonekana wakivuta bangi
wakiwa njiani na tukio hilo kuvuja kwa njia ya video hali iliyopeleka
baadhi ya mashabiki wa shoo yao kuchoma moto tiketi za ziara hiyo.
Chombo kimoja cha habari kimefanikiwa kuidaka video hiyo ya dakika 5
ikionyesha nyota hao wakivuta bangi na kuongea maneno yaliyowakera
baadhi ya mashabiki wao.
Baadhi ya mashabiki walikasirishwa sana na kipande cha video hiyo na
kuwazungumzia mastaa hao kuwa hawajali mashabiki wao ambao wengi ni
vijana na kuwafundisha tabia zisizofaa huku wengine wakiweka picha
mitandaoni wakiwa wanachoma tiketi za shoo hiyo.
0 Comments