Ticker

10/recent/ticker-posts

Ummy Mwalimu Awafungukia Wataalam wa Afya "Punguzeni Semina Mpate Muda wa Kutoa Huduma"

 Ummy Mwalimu Awafungukia Wataalam  wa Afya "Punguzeni Semina Mpate Muda wa Kutoa Huduma"

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, amewataka Wataalamu wa Afya Nchini kupunguza semina ili kuwa na muda zaidi wa kutoa Huduma bora za Matibabu kwa Wananchi


Akiwa katika ziara Mkoani #Simiyu amesema “Wataalamu wa Afya punguzeni semina maana mmekuwa na semina nyingi hadi kusababisha Wagonjwa kukosa Huduma kwa wakati na kumekuwa na msongamano mkubwa katika vituo vya kutolea Huduma za Afya sababu ya semina.”


Aidha, ametoa rai kwa watoa Huduma Nchini kuzingatia utumiaji wa Lugha nzuri, weledi na Maadili na kuzingatia viapo vya Wataalamu wa afya wakati wa kuwahudumia Wananchi

Post a Comment

0 Comments