Ticker

10/recent/ticker-posts

KIKAO CHA KAMATI YA NISHATI CHAFANYIKA OFISI ZA BUNGE DODOMA



 Waziri wa Nishati, Dkt.Medard Kalemani akizungumza katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Nishati. Wizara hiyo iliwasilisha taarifa kuhusu utekelezaji na hali ya upatikanaji wa fedha za Miradi ya Kusambaza Umeme Vijijini (REA).Pembeni yake ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Mhe. Subura Mgalu. Kikao hicho cha kamati kimefanyika katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati, Mhe. Dunstan Kitandula akizungumza katika kikao cha Kamati. Kamati hiyo ilipokea na kujadili taarifa kuhusu utekelezaji na hali ya upatikanaji wa fedha za Miradi ya Kusambaza Umeme Vijijini (REA).Pembeni yake ni Katibu wa Kamati hiyo Felister Mgonja. Kikao hicho cha kamati kimefanyika katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nishati wakiwa katika kikao cha kamati hiyo ambapo walikutana na watendaji wa Wizara ya Nishati na Wakala wa Umeme Vijijni. Kikao hicho cha kamati kimefanyika katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.
 PICHA NA OFISI YA BUNGE


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2QW70Qj
via

Post a Comment

0 Comments