Ticker

10/recent/ticker-posts

WAZIRI SIMBACHAWENE, TAASISI YA SOKOINE WAKUTANA KUTAMBULISHA MRADI WA KUKABILI MABADILIKO YA TABIANCHI


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi kutoka Taasisi ya Kumbukumbu ya Sokoine waliofika ofisini kwake lwa lengo la kuutambulisha Mradi kuimarisha mfumo wa kupanga bajeti na kuhuisha masuala ya mabadiliko ya tabianchi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Fasal Issa alisema Mradi huo wenye thamani ya sh. bilioni 2 utatekelezwa katika wilaya za Mpwapwa, Chamwino na Kondoa mkoani Dodoma.

Alisema kuwa lengo la mradi huo ni kujengea uwezo wilaya hizo katika kuboresha uhimili wa mabadiliko ya tabianchi hususan katika sekta ya maji.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/33hOvtg
via

Post a Comment

0 Comments