Ticker

10/recent/ticker-posts

Viongozi Wateule serikali za vijiji na vitongoji Tandahimba waapishwa

Wateule kwa nafasi mbalimbali za uongozi wa serikali  ngazi ya Kijiji ,vitongoji,Wajumbe mchanganyiko na viti maalum mwaka 2019  wa Wilaya ya Tandahimba wameapishwa leo

Akizungumza  na wateule hao baada ya kuapishwa mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya  Benaya Kapinga aliwaeleza kuwa habari ya siasa inaishia leo kinachofuata ni kufanya kazi 

"Mnatakiwa kwenda kufanya kazi katika maeneo yenu bila kujali itikadi yoyote ya vyama ,dini Wala rangi,kafanyeni kazi wananchi wanataka kuona maendeleo"alisema.

Naye mwezeshaji George Kashura aliwaeleza kuwa wananchi wanataka kujua mapato na matumizi hivyo muwashirikishe wananchi katika shughuli mbalimbali za maendeleo

"Mfanye vikao na wananchi  na msome mapato na matumizi ya fedha zinazoletwa kwa ajili ya maendeleo mbalimbali katika ngazi za vijiji na vitongoji,ili wananchi wajue kinachoendelea,"alisema Kashura
 Wateule kwa nafasi mbalimbali za uongozi wa serikali  ngazi ya Kijiji ,vitongoji,Wajumbe mchanganyiko na viti maalum mwaka 2019  wa Wilaya ya Tandahimba wakiapishwa  leo

 Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya Benaya Kapinga akitoa neno kwa wateule
 Mwezeshaji George Kashura akisistiza wateule Kusoma mapato na matumizi katika vijiji na vitongoji vyao
 Hakimu Mkazi wa Wilaya Joseph Waruku akiwaapisha wateule


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2qNMxCU
via

Post a Comment

0 Comments