Ticker

10/recent/ticker-posts

Tumbi kutumia Sanamu kufanya mafunzo ya Afya kwa Vitendo

Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha Afya cha Kibaha (Kibaha College of Health and Allied Science) wakishuhudia hafla ya makabidhiano ya sanamu. 
Mgeni Rasmi, Dkt. Damian (kushoto), Dkt. Msangi anayefuatia, Balozi Anisa na Dkt. Mwande (kulia) wakikata utepe kuashiria kuanza kutumika kwa sanamu kwa wataalamu wa afya katika kufundishia. 
Sanamu aliyebatizwa jin la Msafriri amezinduliwa rami ili watalamu wa afya wamtumie kufanya mafunzo kw vitendo. 
Dkt. Damian akipokea vitabu vya msaada vyenye thamani ya milioni 30 za Kitanzania kutoka taasisi ya TUHEDA. Vitabu hivyo vitasambazwa kwenye taasisi mbalimbali ikiwemo Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. 
Picha ya Pamoja 
Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani (Tumbi, Kibaha), Dkt. Sylas Msangi akitoa neno la ukaribiho katika hafla ya makabidhiano ya Snamu kwa ajili ya mafunzo ya vitendo kwa wataalamu wa afya. Sanamu hilo limetolewa msaada na Umoja wa Wataalamu wa Afya wa Watanzania wanaoishi Uingereza (Tanzania-UK Healthcare Diaspora Asociation-TUHEDA) 
Mwakilishi wa TUHEDA ambaye ni Mtanzania anayeishi Uingereza na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Sukari, Bw. Nasibu Mwande akiongea machache kuhusu umuhimu wa Snamu kwa wataalamu wa afya katika mafunzo kwa vitendo. 
Mkurugenzi wa Diaspora kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Anisa Mbega akitoa maelezo namna Wizara ya Mambo ya Nje na Balozi za Tanzania zinavyofanya kazi ya kuhamasisha Diaspora waweze kuchangia maendeleo ya nchi yao. 
Meza Kuu ikipiga makofi kuunga mkono maelezo ya Balozi Anisa. 
Mkurugenzi Msaidizi katika Idara ya Tiba kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Caroline Damian ambaye alikuwa Mgeni Rasmi aliyepokea Sanamu kwa niaba ya Serikali. 
Sanamu ambayo, Dkt. Damian alimpokea kwa niaba ya Serikali akiwa anapatiwa matibabu kwa madhumuni ya wataalamu wa afya kujifunza kwa vitendo. Anayetoa maelezo ni mtaalamu kutoka Uingereza ambaye ni rafiki wa Watanzania wanaoishi Uingereza. 
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa katika hafla ya makabidhiano ya Sanamu. 
















from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2pZ52UE
via

Post a Comment

0 Comments