Ticker

10/recent/ticker-posts

KADUGUDA ATEULIWA KUWA KAIMU MWENYEKITI KLABU YA SIMBA

Kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Swedy Mkwabi, Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Simba Sports Club Limited imemteua, Mwina Kaduguda kuwa Kaimu Mwenyekiti wa Klabu hiyo.

Taarifa kwa Umma iliyotolewa mapema leo na Klabu hiyo, imeeleza uteuzi huo umeanza leo Novemba 19, 2019. Tarehe ya Uchaguzi kujaza nafasi ya Mwenyekiti wa Klabu hiyo utatangazwa na Bodi ya Wakurugenzi hapo baadae.

Hata hivyo, Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Simba Sports Club imemteua, Salim Abdallah Muhene kuwa Makmu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni hiyo, kwa uteuzi huo kuanza leo.

Taarifa hiyo imeeleza teuzi hizo zimefanywa kwa mujibu wa Mamlaka ya Bodi chini ya Ibara ya 50 ya Katiba ya Klabu ya Simba yam waka 2018.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/35hqQtr
via

Post a Comment

0 Comments