Ticker

10/recent/ticker-posts

Rapa Snoop Dogg Apewa Heshima ya Hollywood Walk of Fame

Snoop Dogg Apewqa Heshima ya Hollywood Walk of Fame

Rapper  wa Marekani, ‘Snoop Dogg’ amefanikiwa kuungana na mastaa wengine duniani waliowahi kupatiwa heshima ya nyota ya Hollywood Walk of Fame siku ya Jumatutu Nov 19.
Kupata heshima ya nyota hiyo ni ndoto ya kila staa duniani kwa kuwa si kila mtu anaweza kupata nafasi hiyo
Sherehe hiyo ilihudhuriwa na mastaa kama Dr. Dre, Quincy Jones, Pharrell Williams, Ty Dolla $ign, Warren G, na  Jimmy Kimmel ambaye ni mtangazaji maarufu wa televisheni.

Baada ya kupewa heshima hiyo  Snoop alitoa shukrani zake akisema: “Najishukuru sana mimi, kwa kuwa mimi wakati wote.  Snoop Dogg we ni mbaya sana.”

Dr Dre alifunguka kwa kumpongeza Snoop kwa kusema, “Almasi ya kweli inang’aa juu. Snoop ana kipaji cha kweli, Hakuna mtu anayesikika kama Snoop, Staili yake na haiba zilinifanya niamini kwamba ana bahati ya kuja kuwa Superstar