Ticker

10/recent/ticker-posts

HUYU NDIYE ANAYEONGOZA KWA KUWA NA FOLLOWERS WENGI DUNIANI!

Baada ya mtandao wa Instagram kufanya zoezi la kuzifuta akaunti fake Jumatano wiki hii, mwimbaji wa Canada, Justin Bieber alikuwa miongoni mwa mastaa walioathirika kwa kupoteza idadi ya followers milioni 3.5 na kumfanya apoteze sifa ya kuwa mtu mwenye followers wengi zaidi kwenye mtandao huo.Kim Kardashian ambaye pia licha ya kupoteza followers milioni 1.5 kwenye zoezi hilo, lakini amempiku Bieber na kuwa ndiye mtu mwenye followers wengi zaidi katika mtandao huo kwa sasa.
Kwa sasa Kim Kardashian West ana followers 22,298,938, huku Justin Beiber akibaki na followers 20,336,350.