TAASISI ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR),imesema vijana wenye umri wa kuanzia miaka 30 na kuendelea, wanaongoza kwa kutumia dawa za kuongeza nguvu za kiume.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
jana,Mkurugenzi wa NIMR,Dk.Mwele Malecela alisema kwa sasa tatizo hilo
ni kubwa ambalo linawakumba vijana wengi hususan barani Afrika.
Alisema hali hiyo,imesababisha vijana hao kutafuta dawa za
kuongeza nguvu za kiume aina ya Mundex,ili waweze kupunguza ukubwa wa
tatizo hilo.
“Vijana wengi wenye umri wa kuanzia miaka 30 na
kuendelea wana matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume, jambo ambalo
limewafanya kutafuta dawa za kuongeza nguvu ili waweze kuzitumia na
kupunguza ukubwa wa tatizo.
“Tangu tugundue dawa hii, idadi kubwa ya wanaokuja
kununua ni vijana hasa wenye umri wa miaka 30,hali ambayo inaonesha wazi
kuwa tatizo hili linakua kwa kasi,”alisema Dk Mwele.