Picha: Wolper, Kajala na Irene Uwoya
Kama ulikuwa hujui basi naku habarisha, mastaa ambao wameshibana
kwa sasa, namzunguzia wema sepetu pamoja na aunty Ezekiel, hapo awali
waliwahi kuingia kwenye bifu zito kisa kikidaiwa kuwa ni penzi la
aliyekuwa mcheza filamu maarufu nchini, marehemu kanumba. Bifu hilo
lilifikia pabaya ambapo mastaa hao walirushiana maneno makali kwenye
mitandao kila mmoja akimshtumu mwenzie kumuibia bwana ake, bifu hilo
lilidumu kwa mda mrefu, lakini sasa ivi mastaa hao wameshibana na kuishi
kama ndugu, ya kale yamepita tazama yamekuwa mapya.
Unakumbuka kipindi kile kwenye Interview ya zamaradi mketema alipowahoji
irene uwoya na wema sepetu kuhusu bifu lao na jackline wolper? Bifu
lilikuwa zito, ambapo chanzo kinadaiwa kuwa ni mwanaume, warembo hao
walinuniana na kutupiana maneno machafu mitandaoni. Ivi sasa mastaa hao
wanaishi kwa amani na maisha yanaendelea.
|