Ticker

10/recent/ticker-posts

ALI KIBA ANASEMAJE KUHUSU KUFANYA KOLABO NA WASANII WA AFRIKA? STORI IKO HAPA

Kuna time utakuwa unajiuliza maswali kuwa kuna umuhimu gani kwa  wasanii wa hapaTanzania kufanya kolabo na mastaa wa Afrika.
Sasa staa wa Bongo Fleva Ali Kiba amejibu swali lako na kusema;Katika kutangaza muziki inasaidia kiasi fulani lakini sio sana, muziki unaweza ukautangaza hata wewe mwenyewe, mimi binafsi muziki wangu nimeutangaza mbali sidhani kama Afrika hainijui bali inanifahamu sema tu kiukweli video zangu nilizokuwa nafanya hazikuwa katika quality nzuri huo ni ukweli naujua kwa hiyo sasa hivi tuko vizuri katika kujipanga nahakikisha kila kitu kitakuwa poa, hiyo inasaidia sana vile vile kubadilisha muziki na kuutangaza muziki wako katika msanii yoyote  ambaye umemchukua labda wa Congo, Nigeria, Uganda, sehemu nyingine nyingi  ili watu waweza kukusikiliza kwa urahisi na vile vile  ni support kubwa inaonesha jinsi gani una ushirikiano na watu wengine-Alisema.