Ticker

10/recent/ticker-posts

HAWA NDIO MASTAA WATATU WA SOKA WANAOONGOZA KUWA NA FOLLOWERS ZAIDI YA MILIONI 10 KWENYE INSTAGRAM…

Insta
Mitandao ya kijamii ni moja ya njia ya mkato kwa mashabiki kuwafikia mastaa wao, mfano tumeona kwenye Instagram mastaa wakiweka picha, fans wao wanaweka like, comment zao basi wanaenjoy kutumia mitandao kuwa karibu na watu wao.
Kwa upande wa mastaa wa soka duniani, mshambuliaji wa Barcelona na timu ya Taifa ya Argentina, Lionel Messi amesogea kwenye top three ya wachezaji wa soka wenye followers wengi duniani, Messi ana jumla ya followers milioni 10 katika mtandao waInstagram.
Messi anakuwa mchezaji wa tatu duniani kwa kuwa na followers wengi huku akiongozwa na mshambuliaji mwenzake Neymar aliyefikisha followers milioni 15.2 na nafasi ya pili ikishikwa na mwanasoka bora duniani Cristiano Ronaldo ambaye ana watu milioni 12.2
leomessi10M muchas gracias a todos (Thank you very much to all)“– @
Messi aliweka ujumbe huo kwenye ukurasa wake Instagram pamoja na picha yake akiwa amevaa jezi yenye namba kumi mgononi na maneno “MESSi 10 MILLONES”.
Messi
Chanzo:Millardayo.