Stori: Imelda MtemaWALE
matapeli wanaotumia jina la Tanzania Loans, ambao huwadanganya watu
kuwa wanatoa mikopo isiyo na riba, wameingia kwenye akaunti ya msanii wa
filamu, Halima Yahaya ‘Davina’ katika mtandao wa facebook na kuwataka
watu kuchangamkia mikopo hiyo.
Msanii wa filamu, Halima Yahaya ‘Davina’.
“Unajua mpaka sasa watu hawanielewi kabisa mimi, wanajua ni kweli
ndiye niliyeandika kitu hicho, si kweli kabisa maana hata ndugu na
marafiki zangu wamenishangaa sana na wengine kuanza kunisema kwamba
nimeanza mambo ya utapeli,” alisema Davina.
Kampuni hiyo ya kitapeli ya Tanzania Loans, huingia katika akaunti za
watu kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, hasa mastaa na kujifanya
kuwashawishi watu wajiunge katika mikopo hiyo, kitu ambacho siyo kweli.
Wananchi wanaombwa kuwa makini na kamwe wasiamini, ni matapeli hao!