Staa
wa filamu hapa Bongo, Vicent Kigosi ama Ray kwa jina maarufu, ametoa
angalizo juu ya kuibuka kwa wingi Watayarishaji wa Filamu ambao
wamekuwa hawazingatii viwango vya ubora wa kazi na hivyo kuharibu soko
la sanaa hiyo.
Ray
akiwa kama msanii mwenye mafanikio tayari, amesema kuwa, sanaa hiyo
inaendelea kukuwa isipokuwa, Watayarishaji filamu hawa wameongezeka sana
na kuna umuhimu wa wao kufahamu kuwa bila ubora, wanajiharibia wenyewe.
Staa
huyu pia akagusia ujio wa kazi yake mpya inayokwenda kwa jina VIP
ambayo kwa nafasi kubwa itagusia swala ya Utalii kwa Wazawa ambao
wamekuwa nyuma katika swala hili kazi ambayo itatoka mapema mwezi ujao
ikiwa na mastaa wakali kabisa ndani yake
0 Comments