Mkongwe kwenye tasnia ya filamu Bongo, Subrina
Rupia ‘Cathy’ amewalaumu vikali mastaa wa kiume Bongo kuwa ndiyo chanzo
kikubwa cha tasnia kutawaliwa na mastaa wa kike wanaojiuza.Akizungumzia kuhusiana na kuwepo kwa madai ya wasanii wa kike Bongo
Movie kujiuza, Cathy alisema hawezi kuweka wazi kama anawajua wahusika
au la, isipokuwa tatizo lipo kwa wasanii wa kiume wenye majina ambao
hukutana na mademu popote na kuwalazimisha wacheze filamu kutokana na
masilahi yao binafsi.“Penye ukweli lazima tuongee maana sisi zamani haikuwa hivi, msanii anapikwa kambini ndiyo baadaye anapewa nafasi ya kuonekana,sasa siku hizi sivyo, mfano siku moja tulikuwa maeneo ya uwanja wa
ndege kuna mdada akapita ambaye kiukweli muonekano wake siyo kabisa, cha
ajabu kuna msanii wa kiume mkubwa tulikuwa naye akamshobokea na
kumlazimisha acheze filamu yake,” alisema Cathy pasipo kutaja jina la
msanii huyo.
0 Comments