Kwa mara ya kwanza tangu walipomwagana, mastaa wawili Bongo,
Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ wanadaiwa
kuoneana aibu walipokutana laivu.
Mastaa wawili Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ pichani.
Akiwa na mtangazaji mwenzake, Edzen Jumanne, wikiendi iliyopita
Jokate alidaiwa kushindwa kumbana Diamond kwa maswali wakati akimhoji
kwenye kipindi kitakachoruka hewani hivi karibuni kupitia TV1.
Jokate na ‘Diamond Platnumz’ wakipata ukodaki pamoja.
Baadaye Diamond alitupia mtandaoni picha akiwa na zilipendwa wake
huyo hivyo kuibua mjadala mzito kuwa huenda bado wanapendana huku
wenyewe wakipiga kimya.
0 Comments