Ticker

10/recent/ticker-posts

MENINAH: HATUENDANI NA DIAMOND PLTNUMZ


Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Meninah Abdulkareem ‘Meninah’ amefunguka juu ya tetesi zinazoeneo kuwa na uhusiano wa chinichini na Nasib Abdul ‘Diamond’ kwa kusema kuwa siyo levo yake. Akichonga na paparazi wetu, Meninah anayetamba na ngoma ya Pipi ya Kijiti alikanusha na kusema kuwa, wote ni mastaa lakini wametofautiana kwa kiasi kikubwa na kwamba hawezi kuwa naye katika mahusiano ya aina yoyote.
Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Nasib Abdul ‘Diamond’
“Kwanza nilishawahi kukutana naye kwenye shoo tofauti na zote sikuwahi hata kuzungumza naye chochote, ni staa na mimi staa lakini tunatofautiana kuwa yeye yupo juu yangu,” alisema Meninah.

Post a Comment

0 Comments