COMEDIAN mwenye
kofia ya uchungaji kwa sasa, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ hivi
karibuni aliwabomoa mastaa wapenzi Nasibu Abdul ‘Diamond’ na ubavu
wake Wema Sepetu kwa kuwaandikia waraka mzito unaohusiana na maisha yao
ya kila siku.
Komedian , Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’.
Katika
waraka huo, aliouweka kwenye ukurasa wake wa Instagram, Masanja
aliwataka wawili hao kujirekebisha mapungufu yao kama kweli wanapendana
kwa dhati.
Akiuzungumzia
waraka huo baada ya kuvutiwa waya na kachala wa Ijumaa, Masanja alisema
hakuwa na nia mbaya kuwaandikia wapenzi hao kama watu watakavyojaribu
kufikiria, bali alifanya hivyo kiroho safi na hivyo ni wajibu wao
kuukubali au kuukataa.
“Sina
maana hiki nilichokisema lazima wakichukue kama kilivyo, bali wao
wenyewe wanapaswa kuangalia mara mbilimbili ushauri wangu kabla mambo
hayajaharibika,” alisema.
Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akipozi.
Alimtaka
Wema kutambua kuwa mume ndiyo kichwa cha nyumba, kwani kwa mujibu wa
Diamond inaonekana binti huyo hamsikilizi mwenziye.
“Naamini
kabisa kwa mujibu wa muongozo niliousoma kupitia maelezo ya Diamond
kuwa hamsikilizagi, hivyo anatakiwa kuomba msamaha tena na tena, akubali
kubadilika.”
WARAKA WENYEWE HUU HAPA
“Hili swala la Diamond na Wema nadhani Mungu amemhurumia mmoja wapo kati ya hao wawili, kama wangekuwa watu wa kuoana wangeshaoana muda mrefu, uchumba gani mrefu kama wanasomea udaktari? Rafiki yangu Nasibu kama kweli mlipendana kwa dhati hizo kasoro zinarekebishika, maana hakuna mwanadamu aliye sahihi kwani hata wewe Nasibu una mapungufu yako.
“Hili swala la Diamond na Wema nadhani Mungu amemhurumia mmoja wapo kati ya hao wawili, kama wangekuwa watu wa kuoana wangeshaoana muda mrefu, uchumba gani mrefu kama wanasomea udaktari? Rafiki yangu Nasibu kama kweli mlipendana kwa dhati hizo kasoro zinarekebishika, maana hakuna mwanadamu aliye sahihi kwani hata wewe Nasibu una mapungufu yako.
Staa wa filamu na mpenzi wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Wema Sepetu.
Na
wewe dada yangu Wema lazima ujue mume ndiyo kichwa cha nyumba kwa
maelezo hayo inaonyesha haumsikilizagi mwenzio, omba msamaha kila mara
na pia ukubali kubadilika.
Mi
sipendi mkiwa mnaongozana wote kwenye shoo ya usiku, mume anatakiwa
aende kufanya kazi mke abaki nyumbani akirudi mwili umepoa hata ujauzito
unaingia, sasa wote stejini mkirudi miili ya moto si mtazaa popompo
jamanii!!!
CHANZO:GPL
0 Comments