Ticker

10/recent/ticker-posts

VISHOKA WANAOWATAPELI WAFANYABIASHARA ACHENI MARA MOJA:TRA

Irene Donald Meneja msaidizi wa mkoa wa kikodi wa Arusha,Upande wa ukusanyaji wa madeni na ridhaa ya ulipaji kodi.
Mkuu wa wiaya Arumeru Jerry Muro akizungumza katika wiki ya Elimu ya mlipa kodi iliyoandaliwa na TRA Mkoni Arusha.


Na Vero Ignatus,Arusha.

Onyo kali limetolewa kwa Vishoka wanaowatapeli wafanyabiashara kupitia mgongo wa Mamlaka ya Mapato TRA mkoani Arusha waache kufanya hivyo mara moja kwani Mamlaka hiyo itawatachukulia hatua kali za kisheria kwani wanakwamisha ulipaji kodi kwa hiari.

Irene Donald ni Kaimu Meneja wa TRA amesema hayo katika soko la Tengeru alipo alizungumza na walipa kodi katika wiki ya mlipa kodi ,ambapo amesema kuwa kuna baadhi ya watu wanaofahamika kama vishoka ambao hufika TRA na kufanya udanganyifu kwa wafanyabiashara kwa lengo la kujipatia faida huku wakiwaumiza wafanyabiashara.

Jerry Muro ni Mkuu wa Wilaya ya Meru amesema kuwa wafanyabiashara wanapaswa kulipa kodi kwa hiari ili kuchangaia maendeleo ya nchi na kuiwezesha serikali kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi wake.

Baadhi ya wafanyabiashara waliofika kupata elimu ya mlipa kodi Magreth Pallangyo amelalamikia uchafu wa soko la tengeru licha ya kulipa ushuru kwa Halmashauri hiyo hivyo wameiomba serikali itatue changamoto hiyo ili waweze kulipa kodi stahiki.


from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2Q6EQ2I
via

Post a Comment

0 Comments