Baada ya kuwa katika mahusiano yaliyodumu kwa miaka 7 na kufanikiwa kuweka uhusiano wao nje ya macho ya umma, msanii maarufu wa Bongo Kleyah amefunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu ambaye pia ni meneja mshirika, Mhandisi Barnabas Ndyanabo mjini Kampala, Uganda Septemba 10, 2016.
Harusi ilifanyika katika hoteli ya kifahari ya Serena. Sherehe hiyo ilibarikiwa na mualiko wa wageni 100 ambao ni watu wa karibu sana wa familia na marafiki.
Bongo songstress huyo alivalia lulu beaded fascinator na lace Berta vilivyonogesha gauni maalum lililotengenezwa na designer maarufu kutoka nchini Afrika Kusini na lilikuwa kama mermaid silhouette na alivalia viatu vya Bradgley Mischaka.