Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor H. Seff ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa barabara za Mtili- Ifwahi na Wenda- Mgama zinazotekelezwa na Mkandarasi China Henan International Cooperation (CHICO) ambapo awali alianza kazi kwa kusua sua.
Akiwa katika kikao cha pamoja na Mkandarasi, Mhandisi Seff alimtaka Mkandarasi CHICO kuongeza kasi zaidi ili kumaliza kazi kwa muda uliopangwa katika Mkataba na Wananchi watumie barabara hizo ili kujiletea maendeleo na kukuza uchumi wa nchi .
Hata hivyo, akiwa katika Halmshauri ya Mufindi, Mhandisi Seff alitembelea ujenzi wa barabara ya Sawala-Mkonge-Iyegeya inayojengwa kwa kiwango cha lami kwa kutumia teknolojia mbadala ya ujenzi wa barabara inayoitwa ECO Roads.
0 Comments