Ticker

10/recent/ticker-posts

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Ashinda Tuzo hii kubwa Afrika

 

Rais Mstaafu wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete ametunukiwa tuzo ya Kiongozi bora wa mwaka 2023 katika Tuzo za Kiongozi Bora wa Afrika kwa Mwaka 2023 (African Leadership Person of the Year) kama Kiongozi Bora wa Mwaka katika Amani na Usalama Barani Afrika.

Akiongea wakati wa hafla hiyo iliyoandaliwa na Jarida la Uongozi Afrika (ALM), na kufanyika Addis Ababa Nchini Ethiopia usiku wa kuamkia leo March 16,2024, Dkt. Kikwete ameshukuru kwa kutunukiwa tuzo hiyo na kuwasihi Waafrika wote kwenye nafasi za uongozi kutoa kipaumbele kwenye masuala kutatua changamoto zilizopo ikiwemo umasikini, changamoto ya chakula, mabadiliko ya tabianchi, magonjwa, ujinga, migogoro ya kisiasa na vita,

“Ukweli ni kwamba, ni kwa heshima kubwa ninakubali kupokea tuzo hii, naipokea sio tu kwa ajili yangu bali kwa niaba ya Waafrika wengine wengu , wawe ni Viongozi wa kisiasa, wenye ushawishi kiuchumi, Viongozi wa Dini, Wanachama wa vikosi vya usalama, Watumishi wa umma, na Wananchi wa kawaida ambao huamka kila siku na kufanya sehemu yao katika kulifanya Bara la Afrika kuwa sehemu nzuri zaidi
ya kuishi”

Dkt. Kikwete ametunukiwa tuzo hiyo kufuatia mchakato uliojumuisha mapendekezo ya majina pamoja na kura zilizopigwa mtandaoni kwa wale waliopendekezwa, huku Dkt. Kikwete akiibuka na ushindi wa 60% ambapo katika hatua nyingine Mstaafu Kikwete pia amepongeza juhudi zinazofanywa na Afrika katika kupiga hatua kimaendeleo hususani mapinduzi makubwa katika kuboresha elimu.

Watanzania walioshinda tuzo hizo ni wawili ambao ni Dkt. Kikwete pamoja na Jesca Nkwabi ambaye yeye ametunukiwa tuzo ya Kiongozi bora wa mwaka kwenye kundi la Vijana wanaofanya vizuri Barani Afrika.

Post a Comment

0 Comments