Ticker

10/recent/ticker-posts

Benki ya Dunia:Tunampongeza Mtendaji Mkuu TARURA kwa kusimamia vizuri Mradi wa RISE

 

Wataalamu wa Benki ya Dunia wameelezea kuridhiswa kwao na utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji wa Barabara za Vijijini kwa Ushirikishaji na Ufunguaji wa Fursa za Kijamii na Kiuchumi (RISE) unaotekelezwa na Wakala ya Barabara za  Vijijini na Mijini  (TARURA) ambapo wamesema moja ya sababu za matokeo hayo ya utekelezaji yanatokana na usimamizi mzuri wa kazi pamoja na timu nzima ya Utekelezaji.
Akiongea katika kikao kazi cha watumishi wa TARURA wa Mradi wa RISE pamoja na Wawakilishi wa Benki ya Dunia, kilichofanyika  leo jumanne tarehe 05/03/2024 mwakilishi wa Benki ya Dunia Mhandisi Yonas Mchomvu amesema wao kama Benki ya Dunia wameridhishwa na utekelezaji wa mradi wa RISE ambapo wamempongeza Mtendaji Mkuu wa TARURA kwa kuendelea kusimamia vyema Miradi inayotekelezwa na Serikali kwa Ufadhili wa Benki ya Dunia pia aliipongeza TARURA kwa kuwa na mpangilio mzuri wa wataalamu wa kuendesha mradi ikiwa ni pamoja na kuwa na Kitengo cha Mazingira na Jamii.


Naye Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Mhandisi Victor Seff (pichani) akizungumza katika kikao kazi hicho  ameishukuru Benki ya Dunia kwa kuendelea kufadhili miradi mbalimbali ya Barabara inayotekelezwa  chini ya TARURA Nchini.


Akizungumza katika kikao hicho mratibu wa Miradi ya Benki ya Dunia toka TARURA Mhandisi Haumprey Kanyenye (mwenye tai nyeusi) amesema Mradi wa RISE ulianza Novemba 2021 na utakamilika Juni 2027. Mradi wa RISE umelenga kujenga jumla ya kilometa 535 za barabara kwa kiwango cha  lami, kujenga  maeneo korofi ya barabara ili yapitike, na kufanya matengenezo ya barabara ya jumla ya kilometa 23,000km kwa kuwashirikisha wananchi wanaoishi pembezoni mwa barabara husika . Aidha, Mhandisi Kanyenye alieleza uchaguzi wa Mikoa, Wilaya na barabara ambapo Mradi wa RISE unatekelezwa ulizingatia maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa mazao ya kilimo kutoka kwenye Mpango wa Maendeleo wa Kilimo (ASDPII).


Aidha wataalamu hao kutoka benki ya dunia wamipongeza pia TARURA kwa kuweka kipaumbele katikaa kutoa elimu kuhusu masuala ya Ukatili na Unyanyasaji wa Kijinsia(Gender Based Violence)/Sexual Expoitationa and Abuse and Sexual Harrasment(GBV/SEA/SH) 
Akiongea katka kikao hicho Focal Person  wa  masuala hayo ya unyanyasaji wa Kijinsia Sr.Eutropia Eugen amesema wao kama wawakilishi wa TARURA wanamshukuru Mtendaji Mkuu kwa wa TARURA Mhandisi Victor Seff kwa kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha wanakamilisha majukumu yao kwa mujibu wa sheria na ameahidi ataendelea kuhakikisha wanatoa Elimu kwa jamii ya masuala hayo ya jinsia pamoja na elimu kuhusu jamii kujikinga na virusi vya (STD's) na (HIV -AIDS) kwenye Eneo la Miradi ili kuunga Mkono jitihada za Serikali inayoongozwa na Mhe.Samia Suluhu Hassan kuhakikisa jamii inaelimika kwenye nyanja mbalimbali hasa katika maeneo hayo yenye miradi ya maendeleo ikiwepo inayotekelezwa na wafadhili mbalimbali.

Post a Comment

0 Comments