Ticker

10/recent/ticker-posts

EDNA Lameck: Hamasa na Chipukizi UVCCM Taifa tutaenzi mema ya Lowassa


Katibu wa Hamasa na Chipukizi UVCCM Taifa Ndugu Edna Lameck akisaini kitabu cha Maombolezo  Nyumbani kwa Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa Masaki Jijini Dares Salaam  kufuatia kifo cha Waziri Mkuu huyo Mstaafu wa Serikali ya   Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Edward Ngoyai Lowassa aliyefariki Wiki iliyopita jijini Dar esSalaam katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.


Edna Lameck akiwa na Mtoto wa Marehemu Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli Mhe.Fred Lowassa wakijadili jambo baaada ya kufika nyumbani kwao Masaki kwa ajili ya kuwapa pole kwa kufiwa na baba yao ambapo wengine walioambatana na Edna ni baadhi ya Viongozi wa Hamasa wa UVCCM.Ambapo Edna amesema yeye alimfahamu Lowassa kama Kiongozi Mzalendo na Mchapakazi hivyo Vijana wa UVCCM na Tanzania kwa ujumla wana jambo kubwa la Kujifunza  hasa kuenzi yale mema yote toka kwa Marehemu Lowassa kwa maendeleo ya nchi yetu.

Post a Comment

0 Comments