Ticker

10/recent/ticker-posts

Hii ndio MALAIKA VILLAGE: Eneo Jipya Kubwa la Burudani na Matukio lililofunguliwa jijini DODOMA Jana..Soma Hapa

kuendeleza juhudi za Serikali ya awamu ya 6 inayoongozwa na Mhe.rais Dkt.Samia Suluhu Hassan za kuendelea  kuboresha mambo mbalimbali Muhimu Jijini Dodoma,Tayari  wananchi wameunga juhudi hizo mkono kwa kuwekeza katika eneo la Chinangali II lililopo mkabala na Makao makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT kumefunguliwa eneo zuri na bora kwa ajili ya vikao na Mikutano pamoja na michezo ya watoto ambapo limetambulika kwa jina la MALAIKA VILLAGE na uzinduzi wake ulifanyika 

Eneo Hilo linalomilikiwa kwa 100% na wawekezaji wa kitanzania ni moja ya maeneo bora kabisa yaliyofunguliwa jijini dodoma tarehe 1/1/2023 ambapo uzinduzi wake ulihudhuriwa na mamia ya wananchi wa dodoma na viunga vyake huku wakipata burudani kutoka kwa Msanii Maarufu nchini Linex na Bendi yake huku kiingilio kikiwa ni Bure.


baada ya Uzinduzi huo meneja uendeshaji wa eneo hilo Bwana Abubakar Omar amesema Malaika imekuja kubadilisha mambo mengi hasa eneo la burudani na huduma mbalimbali jijini dodoma kwani eneo hilo tayari kwa sasa lina Supermarket,Bar,Ukumbi wa wazi,Swiing Pool,Sauna pamoja na Huduma za Malazi (Executive Rooms/Lodges/Appartments) kwa ajili ya wageni mbalimbali wanaopenda kukaa eneo tulivu kwa ajili ya kazi zao muda wowote kuanzaia siku moja  hadi mwezi hata miezi  mingi kulingana na Uhitaji wa mteja mwenyewe.Pia Siku Chache Zijazo kutakuwa na ATM kwa ajili ya kutoa huduma za Kifedha .

Eneo Hili lina Ulinzi wa kutosha kwa wateja na mali zao,Umeme wa Uhakika,Mandari Nzuri na Huduma zetu ni za Uhakika hivyo mtu yeyote anayetarajia kutembelea Dodoma au aliyepo Dodoma tunamkaribisha na kuhakikishia hatojilaumu kwa kufika Malaika Village kwa ajili ya Huduma Mbalimbali kwani sisi kwetgu Mteja ni Mfalme na ni Muhimu sana kupata maone ya wateja ili kuboresha zaidi huduma zetu,Alimalizia Mejena Uendeshaji Huyo.

Post a Comment

0 Comments