Ticker

10/recent/ticker-posts

Arusha -Tanzania ni ya 8 Duniani kwa maeneo yanayotafutwa zaidi na watalii,Soma zaidi Hapa

Kwa mujibu wa jarida la Tripadvisor' limetaja maeneo 10 duniani yaliyoingia klwenye trnding ya utalii.
Yaani maeneo yanayotafutwa zaidi mtandaoni kwa lengo la utalii, na katika maeneo hayo jiji la Arusha kutoka Tanzania limefanikiwa kuingia 10 na kushika nafasi ya 8.
Orodha hiyo ipo hivi:
Tripadvisor's Top 10 trending destinations in the world, 2022.
1. Mallorca, Spain
2. Cairo, Egypt
3. Rhodes, Greece
4. Tulum, Mexico
5. Dubrovnik, Croatia
6. Ibiza, Spain
7. Natal, Brazil
8. Arusha, Tanzania
9. Göreme, Turkey
10. Santorini, Greece
Kwa bara la Afrika Arusha ikishika nafasi ya kwanza huku Zanzibar ikishika nafasi ya 21 duniani.
Chanzo. Tripadvisor.
Ikumbukwe moja ya jambo lililochochechea sana kutafutwa huku ni Baada ya Uzinduzi wa Filamu ya Royal Tour iliyoongozwa na Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa lengo la kutangaza vivutio mbalimbali vilivyopo nchini kwa ajili ya kukuza na kufungua upya sekta ya utalii jambo ambalo limekuwa na faida na matokeo makubwa tangu kuzinduliwa kwa Filamu hiyo iliyofanyika Nchini Marekani na Tanzania kwa nyakati tofauti tofauti mwaka 2022

Post a Comment

0 Comments