Akizungumza jijini Mbeya
wakati alipokuwa na semina ya uelimishaji jamii kuhusu umuhumu wa kulinda
vyanzo vya maji na kupanda miti, katika mahojiano maalumu kuhusu nini kifanyike
ili kuhakikisha mazingira ya kila siku ya watu na viumbe hai yanakuwa salama Dr.Madoshi
amesema kwa sasa anafurahishwa na juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali kwenye
maeneo mbalimbali zinakofanyka shughuli za kijamii zenye lengo la kuhifadhi
mazingira tofauti na miaka ya nyuma ambapo eneo hilo halikuwa limetolewa elimu
kwa jamii kuhusu umuhimu wake.
Aidha Mhandisi Madoshi amesema
moja ya maeneo yanayotakiwa kuendelea kuwekewa kipaumbele na jamii ni pamoja na
kuhakikisha utunzaji wa mazingira unakuwa jambo endelevu kwani ni moja ya kitu umuhimu
kwa ajili ya Maisha ya kila siku ya viumbe hai.
Ikumbukwe Dkt.
Heladius M. Makene ni mtaalamu wa mazingira na jamii nchini Tanzania,
anayehusishwa na shughuli za usimamizi wa mazingira na maendeleo ya jamii
katika sekta ya miundombinu na madini. Katika eneo la
jamii na mazingira, Dkt.Madoshi amekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu kuhusu uhifadhi wa mazingira,
ikiwa ni pamoja na kampeni ya “Barabara
na Mitaro siyo Jalala,” ambayo inalenga
kuhamasisha wananchi kutunza miundombinu ya barabara kwa kuepuka kutupa taka
ovyo.
Pia Dkt.
Makene pia amehusika katika tafiti kuhusu athari za kijamii na kimazingira za
sekta ya madini nchini Tanzania. Alishiriki katika utafiti uliochapishwa kwenye
jarida la Resources unaoitwa “Calling for Justice in the Goldfields of
Tanzania,” ambapo alishirikiana na watafiti kutoka Clark University. Utafiti
huo uliangazia changamoto zinazowakumba jamii zinazozunguka migodi ya dhahabu,
hususan kuhusu haki za kijamii, mazingira, na ushiriki wa jamii katika maamuzi
Kwa ujumla, na hitimisho ni kwamba pamoja na kuwa mstari wa mbele katika masuala ya
Mazingira bado Dkt. Heladius Makene anaendelea kuwa ni mmoja wa wataalamu wa mazingira nchini wenye
uzoefu mpana katika masuala ya mazingira na maendeleo ya jamii, na mchango wake
unaonekana katika jitihada za kuhakikisha maendeleo ya miundombinu na sekta ya
madini yanazingatia ustawi wa jamii na uhifadhi wa mazingira.
Mwisho.