Ofisi ya Habari ya Vatican imetangaza kuwa kikao cha #Conclave cha kumchagua Papa mpya kitaanza rasmi tarehe 7 Mei.
Maamuzi haya yalifikiwa na Makardinali walioko Roma siku ya Jumatatu, wakati wa mkutano wao wa tano wa Maandalizi (#GeneralCongregation).
Conclave hiyo itafanyika ndani ya Kanisa la Sistine lililopo Vatican, ambalo litafungwa katika kipindi hicho maalum.
Wakati huu, dunia nzima inaelekeza macho Vatican, ikisubiri kwa hamu jina la kiongozi mpya wa Kanisa Katoliki!