Ticker

10/recent/ticker-posts

WAUGUZI TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) WAADHIMISHA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WAGONJWA, NI WA WODI NAMBA TATU


Maafisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Huduma za Uuguzi wa Taasisi hiyo Robert Mallya (aliyevaa safari suti) mara baada ya kumalizika kwa hafla fupi ya kuadhimisha utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa waliolazwa katika wodi namba tatu.
Mkuu wa Kitengo cha Ubora wa Huduma za Afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tulizo Shemu akiwaeleza wauguzi wa wodi namba tatu jinsi ya kuwahudumia wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa moyo ili waweze kujikinga na maambukizi (infection) kwenye eneo ambalo limefanyiwa upasuaji (kidonda) wakati wa hafla fupi ya kuadhimisha utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa waliolazwa katika wodi hiyo.
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Huduma ya Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akiwapongeza wauguzi wa wodi namba tatu kwa upendo waliokuwa nao kwa wagonjwa wanaowahudumia wakati wa hafla fupi ya kuadhimisha utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa waliolazwa katika wodi hiyo.

Msimamizi wa wodi namba ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Afisa Uuguzi Anastazia Moshi akieleza namna wauguzi wa wodi hiyo wanavyofanya kazi ya kuwahudumia wakati wa hafla fupi ya kuadhimisha utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa waliolazwa katika Taasisi hiyo.


Maafisa Uuguzi wa wodi namba wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Ubora wa Huduma za Afya Dkt. Tulizo Shemu na Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Huduma za Uuguzi Robert Mallya wakimkabidhi dawa zilizotolewa na wauguzi wa wodi hiyo Mkuu wa kitengo cha Ustawi wa Jamii Asha Salum kwa ajili ya wagonjwa wasiokuwa na uwezo wa kulipia gharama za matibabu wakati wa hafla fupi ya kuadhimisha utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa waliolazwa katika wodi hiyo.


Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Huduma za Uuguzi Robert Mallya, Mkuu wa Kitengo cha Ubora wa Huduma za Afya Dkt. Tulizo Shemu na Mkuu wa kitengo cha Ustawi wa Jamii Asha Salum wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete wakiwaongoza wauguzi wa wodi namba tatu kukata keki ikiwa ni ishara ya kuonesha upendo kati yao na wagonjwa wanaowahudumia wakati wa hafla fupi ya kuadhimisha utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa waliolazwa katika wodi hiyo.


Afisa Uuguzi wa wodi namba tatu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jumaa Omary akimlisha keki mgonjwa aliyelazwa katika wodi hiyo ikiwa ni ishara ya kuonesha upendo kwa wagonjwa wanaowahudumia wakati wa hafla fupi ya kuadhimisha utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa waliolazwa katika wodi hiyo.


Maafisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Huduma za Uuguzi wa Taasisi hiyo Robert Mallya (aliyevaa safari suti) mara baada ya kumalizika kwa hafla fupi ya kuadhimisha utoaji wa huduma bora kwa wagonjwa waliolazwa katika wodi namba tatu. (PICHA NA: GENOFEVA MATEMU – JKCI)


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/33FwKmR
via

Post a Comment

0 Comments