Ticker

10/recent/ticker-posts

NBC YAZINDUA KAMPENI YA BIMA YA MAGARI KIPINDI HIKI CHA SIKUKUU KWA KUSHIRIKIANA NA SANLAM.

Mkuu wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Elibariki Masuke (kushoto), akikabidhi kadi ya kujazia mafuta ya Total kwa  mteja wa kwanza kukata bima ya gari kupitia huduma za bima za NBC na Sanlam, Danford Robert Buguru wakati wa uzinduzi wa kampeni ya bima ya magari inayowalenga zaidi watumia vyombo vya usafiri katika msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka. Kampeni hiyo inayoendeshwa kwa kushirikiana na Kampuni ya Sanlam imezinduliwa katika kituo cha mafuta cha Total, Mbezi, jijini Dar es Salaam jana. Wanaoangalia ni wawakilishi kutoka NBC, Sanlam na Total.
Mkuu wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Elibariki Masuke (wa tatu kushoto), Mkurugenzi wa Mauzo wa Total, Marieme Sow (kushoto kwake), wakionyesha kadi ya kuwekea mafuta ya Total wakati wa uzinduzi wa kampeni ya bima ya magari inayowalenga zaidi watumia vyombo vya usafiri katika msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka. Kampeni hiyo inayofanyika kwa kushirikiana na Kampuni ya Sanlam imezinduliwa katika kituo cha mafuta cha Total, Mbezi, jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni; Mkuu wa Bima wa NBC, Benjamin Nkaka, Meneja Masoko wa Sanlam, Marco Yambi, Mkurugenzi wa Sheria na Mahusiano wa Total, Marsha Msuya na Meneja Mahusiano Kitengo cha Bima cha NBC, Kuruthum Mwaluwinga.

Mkuu wa Kitengo cha Bima cha Benki ya NBC, Benjamin Nkaka (kushoto), akikabidhi zawadi mbaimbali kwa  mteja wa kwanza kukata bima ya gari kupitia huduma za bima za NBC na Sanlam, Robert Danford Buguru, wakati wa uzinduzi wa kampeni ya bima ya magari inayowalenga zaidi watumia vyombo vya usafiri katika msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka. Kampeni hiyo inayoendeshwa kwa kushirikiana na Kampuni ya Sanlam imezinduliwa katika kituo cha mafuta cha Total, Mbezi, jijini Dar es Salaam jana. Wanaoangalia ni wawakilishi kutoka NBC, Sanlam na Total.
 Mkuu wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Elibariki Masuke (katikati), akisaidia kuweka mafuta ya ofa katika gari la mteja wa kwanza kukata bima ya gari kupitia huduma za bima za NBC na Sanlam, Robert Danford Buguru (kulia), wakati wa uzinduzi wa kampeni ya bima ya magari inayowalenga zaidi watumia vyombo vya usafiri katika msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka. Kampeni hiyo inayoendeshwa kwa kushirikiana na Kampuni ya Sanlam imezinduliwa katika kituo cha mafuta cha Total, Mbezi, jijini Dar es Salaam jana. Nyuma yake ni Mkuu wa Bima wa NBC, Benjamin Nkaka.
Mkuu wa Wateja Binafsi wa Benki ya NBC, Elibariki Masuke (kulia), akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya bima ya magari inayowalenga zaidi watumia vyombo vya usafiri katika msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka. Kampeni iliyozinduliwa na NBC kwa kushirikiana na Kampuni ya Sanlam imezinduliwa katika kituo cha mafuta cha Total, Mbezi, jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni; Mkuu wa Bima wa NBC, Benjamin Nkaka, Meneja Masoko wa Sanlam, Marco Yambi na Mkurugenzi wa Mauzo wa Total, Marieme Sow.
Meneja Chapa na Mawasiliano wa Benki ya NBC, David Raymond (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo ambapo NBC ilizindua kampeni ya bima ya magari inayowalenga zaidi watumia vyombo vya usafiri katika msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka. Kampeni hiyo inayoendeshwa kwa kushirikiana na Kampuni ya Sanlam imezinduliwa katika kituo cha mafuta cha Total, Mbezi, jijini Dar es Salaam jana. 


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/35KLvGX
via

Post a Comment

0 Comments