Ticker

10/recent/ticker-posts

WATU ZAIDI YA MILIONI 100 WANAOTAFUTA HUDUMA ZA AFYA AFRIKA MASHARIKI KUNUFAIKA

App ya  ADA


Simu yako daktari wako....!

Na Mwandishi Wetu
TAKRIBANI watu zaidi ya milioni 100 wanaotafuta huduma za afya nchi za Afrika Mashariki wanatarajia kunufaika na Programu ya kwanza ya kishwahili yenye uwezo wa kutathmini dalili za magonjwa inayoendeshwa na akili bandia (“AI”).

Programu hiyo iliyozinduliwa kwa ushirikiano na Shirika la Fondation Botnar la Uswisi, Global Health Initiative - ADA pamoja na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) cha jijini Dar Es Salaam, Tanzania inatarajiwa kuwa mkombozi kwa jamii hasa za kipato cha chini na kati.

Taarifa zaidi za wadau wa program hiyo zinaeleza kuwa inawezesha upatikanaji wa taarifa za afya na ushauri App, iliyokuzwa na Ada Health, inachanganya hifadhidata ya maarifa bora zaidi ya kitiba duniani na teknolojia erevu ya fikra ili kuwasaidia watumiaji kuelewa nini kinaweza kuwa kinasababisha dalili zao, na pia kuwapa mwongozo maalum kuhusu wanachotakiwa kufanya baada ya hapo.

Programu hiyo ‘app’ inakusudia kuwawezesha wagonjwa kupata taarifa juu ya kinachowasumbua baada ya kuingiza dalili za ugonjwa kisha kufanya maamuzi kuhusu afya zao, huku ikisaidia kutoa huduma za afya zilizopo, madaktari, na kliniki. Ulimwenguni kote kuna watu bilioni 4 - zaidi ya nusu ya idadi ya watu duniani - hawawezi kufikia huduma za msingi za afya.

“Watu bilioni nne duniani kote hawawezi kufikia huduma za msingi za afya, na nchi nyingi zikiwemo Tanzania, Kenya, Somalia na Msumbiji zina daktari chini ya 1 kwa watu 1,000 ,” 2 alisema Hila Azadzoy, Mkurugenzi Mtendaji wa Global Health Initiative ya Ada.

Bi Azadzoy anabainisha; “Kutokana na upokeaji mpana wa teknolojia ya kidijitali, kuna fursa kubwa kwa AI kusaidia kushughulikia hili suala [upungufu wa wahudumu wa afya] kwa kuboresha upatikanaji wa huduma kwa wagonjwa na kuwawezesha madaktari kuwa na athari kubwa zaidi kadri iwezekanavyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Magonjwa ya Watoto wa Chuo Kikuu cha Muhimbili Cha Afya na Sayansi Shirikishi anasema ili kuwa na ufanisi, teknolojia hizi lazima zirekebishwe kulingana na hali za kitiba, kitamaduni, na kilugha katika kila eneo.

Anasema Chuo Kikuu cha Muhimbili kimesaidia maboresho kwa app hiyo ya Kiswahili. “…Tutakuwa tunaendelea kushirikiana na wataalamu wa ndani ya Afrika Mashariki kugundua njia zaidi za kuweza kuboresha uwezekano wa kufikia huduma za afya.”

“Kuna upungufu mkubwa katika huduma za afya ndani ya Afrika Mashariki na itakuwa vigumu sana kushughulikia suala hili kwa kuongeza idadi ya wafanyakazi wa afya na madaktari tu. Tunaweza kutatua hili tatizo na kufanya kila familia iweze kufikia huduma za afya kwa kutumia teknolojia ya kisasa,” alisema, Dk. Salim.

Naye Mkuu Mtendaji wa Fondation Botnar, Dk. Stefan Germann alisema wamefanikisha marekebisho kulingana na magonjwa na dalili zilizoenea zaidi eneo hili, tunapiga hatua muhimu katika kuwaongoza mamilioni ya watu kwenye kutafuta matibabu. AI ina uwezo mkubwa wa kusaidia kuboresha ufanisi na ubora wa mifumo yetu ya afya kupitia huduma ya kibinafsi na ya ubashiri zaidi; tunaamini ni muhimu kwamba faida hizi zinapatikana kwa kila mtu, ulimwenguni kote.

Kasoro za changamoto hii ya afya inawaathiri zaidi watu kwenye nchi zenye kipato cha chini na cha kati. Afrika Mashariki ni ukanda ambao umeathiriwa sana na suala hili. Kwa kutoa programu ya kitiba ya tathmini ya dalili inayoendeshwa na akili bandia kwa Kiswahili, lugha ambayo inatumiwa na zaidi ya watu milioni 100 kwenye nchi kama Tanzania, Kenya, Uganda, Msumbiji, mpaka Somalia, Ada inatumaini kuongeza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa kufikia taarifa bora za afya na ushauri, haswa kwa vijana na familia. Toleo la Kiswahili la app ya Ada limekuzwa kama sehemu ya Mpango wa Afya Duniani, “Global Health Initiative (GHI)” wa Ada.

Huu ni mpango wa muda mrefu wenye lengo la kukabiliana na upungufu wa wafanyakazi katika sekta ya afya - ambao unatarajiwa kufikia zaidi ya milioni 12.9 ifikapo mwaka 2035. Ada inakabiliana na upungufu huu katika huduma za afya.

Dk. Germann, anaongeza kuwa App kama ya Ada inaweza kuwafanya wagonjwa, haswa vijana, kuwa wadau wenye ufahamu juu ya afya zao. Hivyo basi, kuunda vifaa vya afya vya kidijitali maalumu kwa matakwa na mahitaji ya eneo husika katika nchi za kipato cha chini na cha kati ni muhimu katika kufikia usawa kwenye upatikanaji wa huduma za afya.” aliongeza kusema, “Tunajivunia kuzindua toleo la Kiswahili la app ya Ada na tunatarajia kushirikiana zaidi ili kutekeleza maono yetu ya pamoja ya kutumia teknolojia kusaidia wagonjwa, bila kujali wanaishi wapi.”

Kuchanganya akili bandia, utaalamu wa matibabu ya kibinadamu na nguvu ya teknolojia ya kidijitali ili kufikisha huduma za afya na mwongozo kwa wengi. Washirika wa Ada katika kuikuza na kuifanya app iendane na mazingira ya Afrika Mashariki ni shirika la Fondation Botnar la Uswisi, ambalo ni shirika lililojikita kwenye kutumia teknolojia ili kuboresha afya na ustawi wa vijana katika nchi za kipato cha chini na cha kati.

App inapatikana kupitia simu zote za iOS na Android. Kurekebisha AI za Ada kuendana na changamoto za kipekee za kiafya za Afrika Mashariki Ada imefanya kazi na washirika wenyeji, madaktari na mashirika ya afya ili kuhakikisha app inarekebishwa kuendeana na isimu ya lugha, utamaduni na maudhui ya kitiba ya kila eneo.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2KSQRYv
via

Post a Comment

0 Comments