Ticker

10/recent/ticker-posts

VIFURUSHI BIMA YA AFYA YA NHIF HADHARANI, KUZINDULIWA NOVEMBA 28,2019


Na Avila Kakingo , Globu ya Jamii
VIFURUSHI vya Huduma ya afya kwa kutumia Bima ya afya ya mfuko wa taifa wa bima ya afya (NHIF) vyawekwa hadharani ili kila mtanzania aweze kutumia bima hiyo.

Hata hivyo katika taarifa iliyotolewa leo Novemba 26,2019 na mfuko wa taifa wa bima ya afya (NHIF) inaonyesha kuwa vifurushi hivyo vitazinduliwa Novemba 28 katika viwanja vya mnazi mmoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu. 

Taarifa hiyo inaeleza kuwa uzinduzi huo wa vifurushi hivyo utafunguliwa na kampeni ya usajili wa wananchi watakaohitaji kujiunga na vifurushi hivyo ikiwa na upimaji afya bure kwa wananchi.

Vifurushi hivyo kwa mtu binafsi mwenye umri wa miaka 18 hadi 35 kwa kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 192,000, kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 384,000,  kifurushi cha timiza afya shilingi 516,000.

Kwa wenye umri wa miaka 36 hadi 59 kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 240,000, kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 444,000, na kifurushi cha timiza afya ni shilingi 612,000.

Na kwa wenye umri wa miaka 60 na kuendelea kwa kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 360,000 kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 660,000 na kifurushi cha timiza afya ni shilingi 984,000.

Kwa upande wa bima ya Mume na mke tuu kwa wenye umri wa miaka 18-35 Kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 384,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 732,000 ,  kifurushi cha timiza afya shilingi 996,000.

Kwa wenye umri wa miaka 36 hadi 59 kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 456,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 864,000 , na kifurushi cha timiza afya ni shilingi 684,000.

Na kwa wenye umri wa miaka 60 na kuendelea kwa kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 684,000 kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 1,284,000 na kifurushi cha timiza afya ni shilingi 1,906,000.

Hata hivyo kwa mke,mume na watoto mmoja wenye umri wa miaka 18 hadi 35 Kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 504,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 924,000 ,  kifurushi cha timiza afya shilingi 1,272,000.

Kwa wenye umri wa miaka 36 hadi 59 kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 576,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 1,068,000 , na kifurushi cha timiza afya ni shilingi1,464,000.

Hata hivyo kwa mke,mume na watoto wawili (2)wenye umri wa miaka 18 hadi 35 Kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 612,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 1,116,000 ,  kifurushi cha timiza afya shilingi 1536,000.

Kwa wenye umri wa miaka 36 hadi 59 wakiwa na watoto wao wawili kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 696,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 1,272,000 , na kifurushi cha timiza afya ni shilingi1,728,000.

Kuwa makini katika kufatilia hili na kwa mke,mume na watoto watatu (3)wenye umri wa miaka 18 hadi 35 na watoto wao Kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 720,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 1,284,000 ,  kifurushi cha timiza afya shilingi 1,788,000.

Kwa wenye umri wa miaka 36 hadi 59 wakiwa na watoto wao watatu kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 804,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 1,416,000 , na kifurushi cha timiza afya ni shilingi1,980,000.

Hapa ni kwa wale mume na mke na wenye watoto wanne (4) wenye umri wa miaka 18 hadi 35 pamoja na watoto wao Kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 8160,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 1,52,000 ,  kifurushi cha timiza afya shilingi 2,028,000.

Kwa wenye umri wa miaka 36 hadi 59 wakiwa na watoto wao wanne kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 900,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 1,584,000 , na kifurushi cha timiza afya ni shilingi 2,220,000.

Hata hivyo NHIF kwa upande wa mtu binafsi na mtoto mmoja (1) wameweka vifurushi vifuatavyo kwa wenye umri wa miaka 18 hadi 35 Kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 312,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 576,000 ,  kifurushi cha timiza afya shilingi 792,000.

Na Kwa wenye umri wa miaka 36 hadi 59 wakiwa na watoto wao wanne kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 360,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 648,000 , na kifurushi cha timiza afya ni shilingi 888,000.

Pamoja na hayo NHIF kwa Mtu binafsi na mwenye watoto wawili (2)vifurushi vifuatavyo kwa wenye umri wa miaka 18 hadi 35 Kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 312,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 576,000 ,  kifurushi cha timiza afya shilingi 792,000.

Na Kwa wenye umri wa miaka 36 hadi 59 wakiwa na watoto wao wanne kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 360,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 648,000 , na kifurushi cha timiza afya ni shilingi 888,000.

Pamoja na hayo NHIF kwa Mtu binafsi na mwenye watoto watatu (3)vifurushi vifuatavyo kwa wenye umri wa miaka 18 hadi 35 pamoja na watoto, Kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 540 ,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 924,000 ,  kifurushi cha timiza afya shilingi 1,308,000.

Na Kwaupande wa wenye umri wa miaka 36 hadi 59 wakiwa na watoto wa watatu kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 576,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 996,000 , na kifurushi cha timiza afya ni shilingi 1,404,000.

Hata hivyo NHIF kwa Mtu binafsi na mwenye watoto wanne (4)vifurushi vifuatavyo kwa wenye umri wa miaka 18 hadi 35 Kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 636,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 1,092,000 , na kifurushi cha timiza afya shilingi 1,548,000.

Na Kwa wenye umri wa miaka 36 hadi 59 akiwa na watoto wanne kifurushi cha Najali afya premium ni shilingi 672,000 , kifurushi cha wekeza afya premium ni shilingi 1,164,000 , na kifurushi cha timiza afya ni shilingi 1,644,000.

Hata hivyo taarifa hiyo inawakaribisha wananchi wote kwa ujumla kwaajili ya kujiunga katika mfuko huo kwaajili ya kujikinga na bima ya afya kabla ya kuugua kwa uhakika wa matibabu.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2qPEW6G
via

Post a Comment

0 Comments