Ticker

10/recent/ticker-posts

SERIKALI IPO TAYARI KULIPA DENI LA SHILINGI BILIONI 13 KWA WAKULIMA WA KOROSHO

Serikali imesema ipo tayari kulipa Deni la shilingi Bilioni 13 kwa wakulima wa korosho  Wilayani Tandahimba.

Hayo ameyasema Naibu Waziri wa Kilimo Omari Mgumbo wakati akijibu maswali na kusikiliza kero mbalimbali za  wananchi wa Kijiji Cha Nachunyu 

"Msema kweli mpenzi wa Mungu,tulishindwa kuendelea kuwalipa kwakuwa fedha ilituishia,lakini Sasa tumeshapata fedha baada ya kuuza korosho zetu zote tan220,000  kwaiyo fedha tunayo tunauhakika wa kuwalipa wakulima,"alisema Mgumbo

Alisema  serikali inatarajia kulipa madeni kwa wakulima na vibarua Tanzania nzima shilingi Bilioni 89  ambazo zipo.

"Utaratibu utafanyika katika malipo hayo lakini fedha kwa Sasa ipo,sababu tulikuwa tunalipwa kwa malipwani yaani mzigo upakiwe kwenye meli ndipo malipo  yafuaate kwaiyo tumemaliza zoezi hilo ," alisema Mgumbo

Aidha alisema maghala yapo wazi tayari kwa kupokea mzigo mpya hivyo muda wowote  wataanza kupokea korosho kutoka kwa wakulima
 Naibu Waziri wa Kilimo Omari Mgumbo na Mkuu wa Wilaya Sebastian Waryuba akipata maelezo kutoka kwa mkulima Ahmad Ulenje
Naibu Waziri wa Kilimo Omari Mgumbo  akifafanua jambo wakati akijibu maswali na kusikiliza kero mbalimbali za  wananchi wa Kijiji Cha Nachunyu 
,kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya Sebastian Waryuba .


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2VlZgaM
via

Post a Comment

0 Comments