Ticker

10/recent/ticker-posts

Kampuni ya Bima ya Britam yaibuka kidedea kwenye tuzo za bima mwaka 2019

Meneja Mfuko wa Taifa wa Bima wa Afya(NHIF)-Kanda ya Ziwa,Jarlath Mushashu(kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bima ya Britam Insurance Ltd, Raymond Komanga wakionyesha cheti baada ya Britam kutangazwa mshindi wa kampeni bora ya mwaka 2019.Wengine ni wafanyakazi wa kampuni ya Britam.


 Kampuni ya bima yaBritam Insurance Ltd, imeng’ara kwenye tuzo za bima zamwaka 2019 baada ya kutangazwa mshindi wa kampenibora ya mwaka katika tuzo zilizotolewa na Mamlaka yausmamizi wa Bima Tanzania (TIRA).

Tuzo hizo za bima zilizotolewa na TIRA kwakushirikianana Taasisi ya Bima Tanzania (IIT) na kuzinduliwa Mei 21 ikiwa na lengo la kuhamasisha Ubunifu kwenye sekta yabima pamoja na kuchochea ukuaji endelevu.

Tuzo hizo zilizofanyika mapema wiki iliyopitazilihusishavipengele saba huku kampuni ya Britam iking’ara katikakipengele cha kampeni bora ya mwaka.

Akizungumzia ushindi huoMkurugenzi Mtendaji waBritam, Raymond Komanga alisema unatoa hamasa kwakampuni hiyo kuendelea kutoa huduma zenye viwango vyakimataifa pamoja na kukuza huduma hapa nchini.

Tunafurahi kupata ushindi huu na hii inaonyesha jinsigani tunatambulika katika sekta hii ya bima hivyo niwakati muafaka kwetu kuendelea kutoa elimu nakuhamasisha watanzania wengi zaidi kujiunga na hudumahii muhimu,” alisema Komanga.

Kampeni hiyo ijulikanayo kama “Tupo na Wewe” ilianzaAprili hadi Julai mwaka 2019 na imekuwa kampeniiliyoonesha mafanikio kwa jamii kutokana na kutumia njiambalimbali za mawasiliano kuelimisha wananchi juu yaumuhimu wa bima.

Tuzo hizo zilihusisha pia vipengele vingine ikiwamo tuzoya mjasiriamali kijanaTuzo ya kampuni inayosaidia jamiiKampuni bora ya mwaka, tuzo ya bidhaa bora ya kibunifuya bimapamoja na tuzo ya kijana aliyefanikiwa katikatafiti.

Komanga alisema kampeni hiyo ililenga kuelimisha ummajuu ya uwepo wa bima za aina mbalimbali zinazowezakukidhi mahitaji ya mteja katika kila hatua ya maishaikiwamo nyumbagariafya pamoja na bima kwaajili yataasisi na makampuni.
Aidhaalisema ilitumia njia mbalimbali ikiwamo redio namitandao ya kijamii pamoja na kuwahimiza wafanyakaziwake kujikita katika kuwahudumia wateja kwa wakati nakwa ufanisi ili kuleta muamko wa kujiunga na bimanchini. 
Kampeni hiyo ni moja ya mkakati wa kuunga mkonojitihada za Serikali katika kuhakikiha inafikia asilimia 45 ya watu wenye bima ifikapo mwaka 2021.
Huu ni mwendelezo wa kuwa sehemu ya maisha yawateja wetu na kuhakikisha tunawapa haki stahiki wakatiwa maafa kwa haraka na kwa ufanisi,” alisema Komanga.

Hadi mwaka huu kampuni ya Britam Insurance Tanzania ina matawi katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Dodoma, Mbeya pamoja na Mtwara hukuikitarajia kupanua wigo wa huduma katika siku zijazo.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2pwvLHl
via

Post a Comment

0 Comments