Ticker

10/recent/ticker-posts

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, PHAUSTINE KASIKE AFANYA UKAGUZI GEREZA LINDI NA KINGURUNGUNDWA

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa pili toka kulia) akikagua Bustani ya Gereza Kingurungundwa alipotembelea jana Oktoba 18, 2019.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa pili toka kushoto)akikagua mifuko ya saruji ambayo imenunuliwa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi wa Jeshi hilo sambamba na ujenzi wa Ofisi ya Magereza Mkoani Lindi. Kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Lindi, ACP. Josephine Semwenda.
Mradi wa tofali za “interlock” katika gereza la Lindi. Tofali hizo zinatumika katika ujenzi wa nyumba za Maafisa na Askari katika gereza hilo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Rais kuhusu kutatua tatizo la nyumba za watumishi wa Jeshi hilo kwa kutumia wafungwa pamoja na fursa zilizopo.







Msafara wa Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike, ukipita katika Gadi maalum ya heshima iliyoandaliwa na askari wa Jeshi hilo alipofanya ziara yake ya kikazi katika Magereza mawili ya Mkoa wa Lindi, jana Oktoba 18, 2019 kabla ya kurejea jijini Dar e salaam kuendelea na majukumu mengine ya Kitaifa.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akisalimiana na Mkuu wa Gereza Lindi, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Leonard Chintowa alipowasili jana Oktoba 18, 2019 katika ziara yake ya kikazi Mkoani Lindi.

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(katikati aliyeketi) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa na askari wa Gereza Kingurungundwa(waliosimama)alipotembelea gereza hilo jana Oktoba 18, 2019. Kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Lindi, ACP. Josephine Semwenda na kulia aliyeketi ni Mkuu wa Gereza hilo SP. Eden Bilalo (Picha zote na Jeshi la Magereza).



from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2MTVDVD
via

Post a Comment

0 Comments