Ticker

10/recent/ticker-posts

BRELA KURASIMISHA HUDUMA ZA BIASHARA JIJINI DODOMA

Kaimu Mkurungezi Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Emanuel Kakwezi akizungumza

WAKALA wa Usaji wa Biashara na Leseni nchini (BRELA) unatarajiwa kutoa huduma za urasimishaji wa biashara Octoba 18 na Octoba 19 Jijiji Dodoma kwenye ukumbi wa Chuo cha Mipango Dodoma wakati wa Fursa 2019

Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Mkurungezi Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) Emanuel Kakwezi ambaye pia alifanya ukaribisho kwa wana Dodoma alisema watatoa huduma mbalimbali wakati wa fursa 2019 huku wakiwataka wakazi wa mkoa huo kuchangamkia fursa hiyo muhimu

Alisema kwamba huduma ambazo zitatolewa wakati wa Fursa Dodoma ni usajili wa Majina ya Biashara, Kampuni, Nembo za Biashara na huduma, Hataza, Leseni Daraja A, 
Leseni za Viwanda.

Kaimu Mkurungezi Mkuu alisema wameamua kishiriki kwenye Fursa mwaka huu kutokana uhitaji wa wananchi juu ya ujarasimishaji Biashara zao Pia wameamua kushiriki kutokana na kauli mbiu ya mwaka huu inayosema “Leta Solution” ikiwa kama Taasisi ya Brela ni moja ya solution kwenye Biashara na ubunifu wa wasajiriamali ili kuendana na Serikali ya Viwanda ya sasa

Kikubwa zaidi kilichofanya kushiriki ni kuwafikia wananchi kwa ukaribu 
zaidi na kuwahidumia kwa ukaribu zaidi

Kakwezi alisema Brela pia itashiriki kwenye Fursa mikoa yote ambayo imebaki baada ya Dodoma na watakuwa wanatoa huduma zote zinazotolewa na Brela, ambapo mikoa hiyo ni Tanga, Arusha na Dar Es Salaam 

Hata hivyo alitoa rai kwa wananchi wote kutumia fursa hii ili kuweza kupata huduma za Brela kwani kutakuwa na team ya Brela ambayo itatowa huduma zote na wananchi watakao kidhi masharti kama ya kuwa na Namba ya Kitambulisho cha NIDA na vingezo vingine wataweza kuondoka na vyeti vya Usajili


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2nQZzhp
via

Post a Comment

0 Comments